Raila Odinga na kitendawili cha uenyekiti wa Umoja wa Afrika

Raila Odinga na kitendawili cha uenyekiti wa Umoja wa Afrika

Mwanasiasa huyo ameweka wazi nia yake ya kuwania uenyekiti wa tume ya ya Umoja wa Afrika.
Mwanasiasa huyo mkongwe anaweza kupoteza sifa ya kuwania uenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika(AU) iwapo muswada wa mapendekezo utapitishwa./Picha: Reuters

Na Kevin Philips Momanyi

Kiongozi wa muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga atalazimika kusubiri hatma ya mapendekezo na mabadiliko katika utaratibu wa kumchagua mrithi wa Moussa anayemaliza muda wake kama mwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika, baadae mwaka huu.

Mabadiliko hayo yanaziondolea sifa nchi wanachama wa AU zilizowahi kushika nafasi za uenyekiti na makamu mwenyekiti, kati ya mwaka 2002 mpaka leo.

Chaguzi hizo zitafanyika kwenye mkutano wa AU, mwaka 2025.

Mbali na Kenya, nchi nyingine inayosubiria maamuzi ya wakuu wa AU ni Rwanda, ambayo ilitoa makamu mwenyekiti kwenye umoja huo.

Ndoto za Waziri Mkuu huyo wa zamani wa Kenya zitayeyuka iwapo mapendekezo hayo yatapitishwa na wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika.

Erastus Mwencha, kutoka Kenya, alihudumu katika Umoja wa Afrika, kama makamu mwenyekiti, kati ya mwaka 2008 hadi 2017.

Tume ya Umoja wa Afrika imekuwa na utaratibu wa kupokezana nafasi ya uenyekiti kwa mzunguko kulingana na maamuzi yake ya mwaka 2018, na kwa sasa, zamu ilidondokea katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Raila Odinga ameungwa mkono kwenye nia yake, sio tu na Rais William Odinga, bali pia kiongozi wa Uganda, Yoweri Museveni./Picha: TRTAfrika

Hatua hii inakuja wakati Odinga ameungwa mkono na Rais wa Kenya, William Ruto na Yoweri Museveni kutoka Uganda na kiongozi wa zamani na mwanasiasa mkongwe barani Afrika, Olusegun Obasanjo wa Nigeria.

TRT Afrika