Senegal inashika nafasi ya pili, Misri inashika nafasi ya tano na Cameroon nafasi ya saba katika soka la Afrika, kwa mujibu wa FIFA. / Picha: TRT Afrika

Morocco inaendelea kuongoza Afrika kama timu ya soka ya wanaume iliyoorodheshwa zaidi barani humo, kulingana na viwango vya hivi punde vya FIFA vilivyotolewa Alhamisi.

Washindi wa nusu fainali ya Kombe la Dunia la FIFA 2022 wameorodheshwa katika nafasi ya 13 ulimwenguni, nyuma ya Argentina, Ufaransa, Brazil, England, Ubelgiji, Ureno, Uholanzi, Uhispania, Italia, Kroatia, USA na Mexico kwa mpangilio huo.

Morocco ilikuwa na pointi 1658.49, pointi 5.45 nyuma ya Mexico iliyo nafasi ya 12.

FIFA hutumia fomula changamano ya kukokotoa pointi ambayo ilifanyiwa marekebisho Septemba 2023.

Kwa maneno rahisi, shirikisho la soka duniani hupanga timu kulingana na jumla ya pointi zilizopatikana katika mechi za mashindano katika kipindi fulani.

Tano bora

Wachezaji wa timu ya Morocco wakirudi mjini baada ya kushiriki katika kombe la Dunia mwaka 2022 

Kwa hivyo, timu iliyo na viwango bora imekuwa na matokeo mazuri katika siku za hivi karibuni ikilinganishwa na ile iliyo na nafasi ya chini.

Mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2021 Senegal wanashika nafasi ya pili barani Afrika, na nafasi ya 20 duniani kote, wakiwa na pointi 1600.82.

Tunisia, ambayo inashika nafasi ya 32 duniani, iko nafasi ya tatu barani Afrika ikiwa na pointi 1516.14.

Taifa hilo la Afrika Kaskazini linafuatwa na majirani zake Algeria, ambao wapo katika nambari 33 duniani, wakiwa na pointi 1512.9.

Misri inamaliza timu tano bora za soka barani Afrika, ikiwa na pointi 1511.95, na kuwaweka katika nafasi ya 35 duniani.

Burkina Faso yatinga 10 bora

Nigeria ni ya sita barani humo na ya 40 duniani ikiwa na pointi 1490.48.

Cameroon iko nafasi ya saba barani Afrika na ya 43 duniani ikiwa na pointi 1466.98, ikifuatiwa na Mali iliyo katika nafasi ya 47 duniani kwa pointi 1449.75.

Wenyeji wa AFCON 2023 Côte d'Ivoire - au Ivory Coast - wako katika nafasi ya tisa barani Afrika, na ya 52 ulimwenguni kwa alama 1439.17.

Burkina Faso, ambao wameorodheshwa katika nafasi ya 56 duniani kote, wanakamilisha timu kumi bora za soka barani Afrika kwa pointi 1410.59.

Eritrea haijaorodheshwa

Timu zote za Afrika ziliorodheshwa na FIFA, isipokuwa Eritrea, ambayo shirikisho la soka duniani linasema, ilishindwa kucheza mechi za kawaida.

"Hakuna nafasi (kwa Eritrea) kutokana na kutocheza angalau mechi moja katika kipindi cha miezi 48 iliyopita au kutocheza angalau mechi tano dhidi ya timu zilizoorodheshwa rasmi," FIFA ilisema Alhamisi.

Ifuatayo ni orodha kamili ya viwango vya timu za Kiafrika na FIFA kufikia Oktoba 2023:

1. Morocco (13 duniani kote)

2. Senegal (20)

3. Tunisia (32)

4. Algeria (33)

5. Misri (35)

6. Nigeria (40)

7. Cameroon (43)

8. Mali (47)

9. Côte d'Ivoire (52)

10. Burkina Faso (56)

11. Ghana (60)

12. Afrika Kusini (64)

13. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (65)

14. Cape Verde (74)

15. Guinea (80)

16. Zambia (81)

17. Gabon (86)

18. Uganda (90)

19. Guinea ya Ikweta (91)

20. Benin (93)

21. Mauritania (101)

22. Jamhuri ya Kongo (106)

23. Madagascar (108)

24. Kenya (110)

25. Guinea-Bissau (110)

26. Msumbiji (113)

27. Namibia (114)

28. Angola (116)

29. Gambia (117)

30. Togo (119)

31. Tanzania (121)

32. Sierra Leone (122)

33. Malawi (123)

34. Zimbabwe (125)

35. Libya (126)

36. Jamhuri ya Afrika ya Kati (127)

37. Komoro (128)

38. Niger (129)

39. Sudan (130)

40. Rwanda (140)

41. Burundi (142)

42. Ethiopia (143)

43. Eswatini (zamani Swaziland) - 146

44. Botswana (148)

45. Liberia (151)

46. Lesotho (153)

47. Sudan Kusini (167)

48. Mauritius (177)

49. Chad (179)

50. Sao Tome na Principe (186)

51. Djibouti (189)

52. Ushelisheli (195)

53. Somalia (196)

TRT Afrika