Safari ya ajabu ya Osimhen ilimwezesha kuzuia ushindani mkali kutoka kwa beki wa pembeni wa Morocco Achraf Hakimi na mshambuliaji wa Misri Mohammed Salah./ Picha : CAF 

Victor Osimhen wa Nigeria na Asisat Oshoala walishinda tuzo kubwa zaidi za kibinafsi katika Tuzo za CAF 2023 katika jiji la Morocco la Marrakech Jumatatu usiku, 11 Desemba 2023.

Osimhen, mshambulizi wa Nigeria ambaye aligonga vichwa vya habari nchini Italia na pia kwa mchango wake katika jezi ya Super Eagles, alishinda Mchezaji Bora wa Afrika wa CAF kwa mara ya kwanza huku mtani wake, Oshoala akishinda rekodi yake ya sita ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa CAF wa Wanawake wa Afrika.

Safari ya ajabu ya Osimhen ilimwezesha kuzuia ushindani mkali kutoka kwa beki wa pembeni wa Morocco Achraf Hakimi na mshambuliaji wa Misri Mohammed Salah.

Nyota wa Nigeria, Oshoala ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa CAF kwa Wanawake kwa mara ya sita. Ubabe wa mshambuliaji huyo uliendelea huku akiipaisha Barcelona kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa, na kumaliza kama mfungaji bora wa klabu hiyo akiwa na mabao 27 katika michuano yote.

Kocha Bora wa Mwaka (Wanaume): Walid Regragui (Morocco)/ Picha : CAF 

Walid Regragui wa Morocco alitawazwa kuwa Kocha Bora wa Mwaka wa CAF katika kitengo cha Wanaume - akitambuliwa kwa kuiongoza Simba ya Atlas hadi mkimbio wa kihistoria wa nusu fainali ya Kombe la Dunia nchini Qatar.

Desiree Ellis wa Afrika Kusini alipata tuzo ya Kocha Bora katika kitengo cha wanawake kwa kazi yake bora akiwa na Banyana Banyana. Hii ilikuwa tuzo ya nne ya Ellis katika kitengo hiki, ambayo ameshinda mara kwa mara tangu 2018.

Katika shindano la klabu CAF , Percy Tau wa Afrika Kusini na Al Ahly alishinda Mchezaji Bora wa Mwaka wa vilabu CAF.

Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka (Wanaume): Lamine Camara (Senegal, Metz) / Picha : CAF 

Mchezaji wa Senegal Lamine Camara, mshambuliaji wa FC Metz mwenye umri wa miaka 19, alishinda tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa CAF, kuashiria kupanda kwake kwa daraja katika soka la Afrika.

Bingwa wa Morocco Nesryne El Chad alishinda tuzo ya kwanza ya CAF ya Mchezaji Bora wa Kike Kijana wa Mwaka.

Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka (Wanawake): Nesryne El Chad (Morocco, Lille) / Picha : CAF

Morocco ilishinda tuzo ya Timu ya Taifa ya Wanaume kufuatia uchezaji wao katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022, huku Nigeria ikishinda tuzo ya Timu ya Taifa ya Mwaka ya Wanawake.

Miamba wa Misri, Al Ahly walinyakua tuzo ya Klabu Bora ya Kiume ya Mwaka, huku tuzo ya wanawake ikienda kwa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.

Afrika Kusini ilitawala wachezaji bora wa XI wa bara katika Kitengo cha Wanawake huku wachezaji wawili wa timu ya Morocco ya nusu fainali ya Kombe la Dunia wakijumuishwa katika toleo la wanaume.

Washindi wa mwisho katika kila kategoria waliamuliwa kupitia mchakato wa upigaji kura uliohusisha jopo linalojumuisha Kamati ya Kiufundi ya CAF, Makocha Wakuu, Manahodha wa Timu ya Taifa na wataalamu wa vyombo vya habari.

Orodha ya washindi

  • Mchezaji Bora wa Mwaka (Wanaume): Victor Osimhen (Nigeria, Napoli)

  • Mchezaji Bora wa Mwaka (Wanawake): Asisat Oshoala (Nigeria, Barcelona)

  • Mchezaji Bora wa Mwaka wa Klabu (Wanaume): Percy Tau (Afrika Kusini, Al Ahly)

  • Mchezaji Bora wa Mwaka wa Klabu (Wanawake): Fatima Tagnaout (Morocco, AS FAR)

  • Kocha Bora wa Mwaka (Wanaume): Walid Regragui (Morocco)

  • Kocha Bora wa Mwaka (Wanawake): Desiree Ellis (Afrika Kusini)

  • Kipa Bora wa Mwaka (Wanaume): Yassine Bounou (Morocco, Al Hilal)

  • Kipa Bora wa Mwaka (Wanawake): Chiamaka Nnadozie (Nigeria, Paris FC)

  • Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka (Wanaume): Lamine Camara (Senegal, Metz)

  • Mchezaji Bora Chipukizi wa Mwaka (Wanawake): Nesryne El Chad (Morocco, Lille)

  • Timu ya Taifa ya Mwaka (Wanaume): Morocco

  • Timu ya Taifa ya Mwaka (Wanawake): Nigeria

  • Klabu Bora ya Mwaka (Wanaume): Al Ahly (Misri)

  • Klabu Bora ya Mwaka (Wanawake): Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini)

TRT Afrika