Diamond Platnumz (kulia) ametajwa kuwania tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika nyingi zaidi katika kanda. Picha: Diamond Platnumz

Afrika Mashariki iliibuka na muziki ulioongoza chati mwaka wa 2023, huku kampuni kubwa ya Spotify ikitoa sifa kwa wasanii wa Afrika Mashariki katika ‘Ripoti Iliyokamilika ya 2023’ kwa kuinua kiwango cha juu na kuwavutia wasikilizaji wa ndani na nje ya nchi kwa muziki wao wa ajabu na ushirikiano wao.

Sekta ya muziki ya Afrika Mashariki ni maarufu kwa aina yake ya muziki wa mijini, ambayo kimsingi ni chipukizi la muziki wa pop wa magharibi, haswa hip hop na funk.

Pia kuna ushawishi mkubwa wa nyimbo za kitamaduni za Kiafrika, ambazo ni muziki wa Boomba, unaojulikana pia kama Kapuka nchini Kenya.

Genge, aina ya mtindo wa muziki wa ukumbi wa Afro-dance kutoka Kenya, na mtindo wa muziki wa Bongo Fleva, ambao ni mchanganyiko wa muziki wa wa Marekani na mtindo wa muziki wa asili wa Kitanzania.

Data kutoka kwa tovuti nyingi za streaming wa muziki katika muhtasari wao wa 2023 zimewapa tuzo ya umaarufu Afrobeats kutoka Afrika Magharibi, lakini wasanii wa Afrika Mashariki pia wamejitokeza kwa wingi katika chati tofauti zinazovuma.

Diamond Platnumz

Naseeb Abdul Juma, anayefahamika kwa jina la kisanii Diamond Platnumz, ni mmoja wa wasanii waliouza sana nchini Tanzania, akiwa na jumla ya streams milioni 65 kwenye jukwaa la Spotify mnamo 2023.

Diamond Platnumz

Hii ni zaidi ya mara mbili ya idadi aliyopata mwaka 2022 (milioni 30), akiwa na wasikilizaji milioni 1.4 kila mwezi.

Wimbo wake, Jugni, umesikilizwa na zaidi ya watu milioni 13 na wasikilizaji zaidi ya milioni 1.3 kila mwezi. Nyimbo zake kali zaidi kufikia sasa ni kolabo zake kwenye wimbo wa 'Yope Remix', aliofanya na rapa kutoka Kongo Innoss'B, na kutazamwa zaidi ya milioni 220 kwenye Youtube.

Sauti Sol

Bendi ya muziki ya Sauti Sol ya Kenya ilivunja mioyo yao mnamo Mei 2023 ilipotangaza kuwa wangeacha muziki kwa muda usiojulikana baada ya kutwa pamoja kwa miaka 18.

Waliendelea kusema watafanya ziara na matamasha ya kuaga katika bara hilo na katika baadhi ya nchi za magharibi.

Sauti Sol wameimba pamoja kwa miaka 18. Picha: Sauti Sol

Habari hizo zilizidisha umaarufu wao, huku nyimbo zao zikiruka hadi juu ya chati katika mitandao kadhaa ya streaming.

Spotify, katika ripoti yao, walisema kuwa bendi hiyo ilikuwa na wasikilizaji zaidi ya 400,000 kila mwezi, na wimbo wao wa mwisho, Lil Mama, uliotolewa Novemba 2022, unapiga streams zaidi ya milioni 3 tangu kutangazwa kwa mapumziko wao uliokusudiwa, kulingana na Spotify.

Wimbo wa bendi ya Sauti Sol, Bien Aime-Baraza, ‘My baby’ akimshirikisha Ayra Starr wa Nigeria pia unazidi kupata idadi kubwa, ikiwa na streaming zaidi ya milioni saba mwaka wa 2023 kwenye Spotify. ​

Harmonize

Rajab Abdul Kahali, anayejulikana pia kwa jina la kisanii la Harmonize, ni msanii wa muziki wa Bongo Flava na mjasiriamali kutoka Tanzania.

Harmonize

Wimbo wake, unaoitwa 'Single Again', uliotolewa Agosti 2023, umekuwa na mafanikio, na zaidi ya mitiririko milioni 8 kwenye Spotify. Ushirikiano wake kwenye wimbo mmoja na mwimbaji wa Nigeria Ruger umeangaliwa zaidi ya mara milioni 4 kwenye Youtube.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 33 ana zaidi ya wasikilizaji 760 000 kila mwezi kwenye Spotify, pamoja na ushirikiano wake na Blag Jerzee (Falling for You) uliotolewa mwaka 2021 bado ni kipenzi kikuu cha mashabiki mnamo 2023 na mitiririko streaming ya milioni 34.

Rayvanny

Raymond Mwakyusa, anayejulikana na mashabiki kama Rayvanny, ni mwimbaji wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 30 mwenye streams zaidi ya milioni 100 kwenye Boomplay na zaidi ya usikilizaji 500,000 wa kila mwezi (Spotify) na kustream milioni 128 kwa nyimbo zote (Spotify).

Rayvanny  MTV Awards 2021 Tuzo

Wimbo wake 'Melody', akimshirikisha mwimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka Tanzania Jay, umetazamwa zaidi ya milioni 10.1 kwenye TikTok.

Rayvanny anajulikana kwa utumiaji wake mzuri wa autotune kutoa mchanganyiko wa muziki wa Taarab -Bongo.

Rayvanny aliibuka kidedea baada ya kutoa wimbo wake wa kwanza “Kwetu” mwaka wa 2019. Wimbo wake wa “Tetema” aliomshirikisha Diamond Platnumz ulizidi kumtia nguvu kwenye anga ya muziki wa Afrika Mashariki. ​

Xenia Manasseh

Xenia Manasseh ni mwanamuziki anayekuja kwa kasi wa R&B wa Kenya ambaye anaingia kwenye orodha yetu kwa nguvu za ajabu za wasichana.

Xenia Manasseh

Mwenye umri wa miaka 26 ana wastani wa wasikilizaji zaidi ya 300,000 kila mwezi, na wimbo wake ‘When It’s Over’’ uliotolewa mwaka wa 2019 una streams zaidi ya milioni moja, kulingana na Spotify 2023 wrap.

Ushirikiano wake na msanii kutoka Kenya Ukweli katika wimbo wa ‘Love or Leave me’ umepata streams zaidi ya milioni 1.2 kwenye Spotify. ​

TRT Afrika