Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Rais wa Benki ya Dunia Ajay Banga. Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia.

Abiy Ahmed alielezea mageuzi ya jumla ya kiuchumi yanayoendelea na maendeleo ya ajenda ya mageuzi ya kiuchumi ya Ethiopia.

Wakati wa mkutano wa nchi hizo mbili pamoja na wajumbe wao, Waziri Mkuu alitoa muhtasari wa mageuzi ya jumla ya kiuchumi yanayoendelea pamoja na maendeleo yaliyopatikana katika ajenda ya mageuzi ya kiuchumi ya Ethiopia.

Viongozi hao wawili walitembelea viwanda viwili viliyopo ndani ya Hifadhi ya Viwanda ya Bole Lemi kabla ya kupanda miche ya Green Legacy.

Kwa upande wake, wakati akiwa Addis Ababa, Banga pia alikutana na maafisa wa serikali, akiwemo Waziri wa Fedha Ahmed Shide, na Mamo Mihretu, Gavana wa Benki ya Taifa ya Ethiopia.

Mojawapo ya kiwanda cha utengenezaji wa nguo na viatu nchini Ethiopia. Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia.

"Mafanikio ya Ethiopia katika suala la kutoa ajira na uhusiano wa soko yanatia matumaini". Rais wa Benki ya Dunia Ajay Banga alisema.

"Benki ya Dunia ni muhimu kwa ukuaji wetu wa uchumi katika kupanua wigo wake wa ushirikiano na Ethiopia kwa kuongeza ufadhili wenye masharti mepesi, ufadhili thabiti wa uwekezaji kupitia Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC), na msaada kwa ajenda yetu ya mageuzi ya uchumi wa nyumbani." Abiy Ahmed alisema.

Hivi majuzi, Wizara ya Fedha ya Ethiopia na Benki ya Dunia zilisaini Mkataba wa ufadhili wenye thamani ya dola za Marekani milioni 400 ambapo Dola za Marekani Milioni 350 kati ya hela hizo ni ruzuku huku Dola Milioni 50 ikiwa ni mkopo.

TRT Afrika