Sekta nyingine ambazo zitafaidika kutokana na ushirikiano ni nishati, sanaa, masuala ya vijana na utalii. / Picha: ikulu Kenya

Rais Ruto yuko nchini Djibouti kwa ziara ya siku mbili kabla ya mkutano wa marais wa Mamlaka ya Kiserikali ya Maendeleo (IGAD) utakaofanyika Jumatatu.

Akizungumza wakati wa kikao na wanahabari katika Ikulu ya Rais ya Djibouti siku ya Jumapili, Ruto alisema hatua hiyo itaruhusu watu kusafiri huru ili kuimarisha biashara kati ya nchi hizo mbili.

"Nimejitolea kwa dhati kuondoa vizuizi vilivyowekwa na mahitaji ya visa kwa raia wa Djibouti wanaosafiri kwenda Kenya. Kwa hivyo, Kenya imehitimisha taratibu zinazohitajika kuwezesha ziara bila visa kwa raia wa Djibouti hadi Kenya."

Rais William Ruto ni mwenyeji wa Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh . / Picha:ikulu Kenya 

Ruto, hata hivyo, hakufichua katika taarifa yake ni lini uingiaji nchini Kenya bila visa kwa raia wa Djibouti utaanza kutekelezwa.

Chini ya sheria za sasa za uhamiaji, raia wa Djibouti wanahitaji nakala ya hati ya kusafiri nje ya nchi, picha ya pasipoti, uthibitisho wa mahali pa kulala na uthibitisho wa kusafiri ili kupata visa ya Kenya.

Ndege za moja kwa moja

"Kurejeshwa kwa muunganisho wa anga bila shaka kutakuwa na athari kubwa katika kuimarisha biashara kati ya mataifa yetu mawili," alisema.

Alisema pia Kenya inafanya kazi kwa karibu na Djibouti katika sekta ya elimu, na kuahidi kuwaruhusu wanafunzi 300 wa Djibouti kujiunga na vyuo vikuu vya Kenya. Alisema wanafunzi hao wa kigeni watalipa karo sawa na Wakenya.

Sekta nyingine ambazo zitafaidika kutokana na ushirikiano wa nchi hizo mbili ni nishati, sanaa, masuala ya vijana na utalii.

Rais Ruto alisema Djibouti imeruhusu kampuni ya nishati ya Kenya kuchimba visima viwili vya jotoardhi nchini, huku awamu ya kwanza ya mradi ikiwa tayari imekamilika.

Mzozo wa Sudan

Akizua wasiwasi kuhusu vita vinavyoendelea nchini Sudan, Ruto alisema serikali za Kenya na Djibouti zimekubaliana kushirikiana na Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir "kutayarisha pendekezo madhubuti la kusaidia kumaliza mzozo kabla ya Mkutano wa 14 wa Kawaida wa Bunge la IGAD.

Ruto ni mwenyeji wa Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh.

Majadiliano kuhusu vita vinavyoendelea nchini Sudan yanatarajiwa kujitokeza/Picha:ikulu Kenya

Rais Guelleh katika hotuba yake Jumapili alisema serikali yake na Jamhuri ya Kenya "zinashiriki uhusiano wa baraka wa mshikamano, ushirikiano na urafiki, unaosukwa na historia na mali ya pamoja ya eneo moja".

Majadiliano kuhusu vita vinavyoendelea nchini Sudan yanatarajiwa kufanyika wakati wa mkataba wa IGAD huku mataifa ya Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika yakitafuta kumalizika kwa vita kwa amani.

Sudan, iliyokumbwa na mzozo, ni nchi mwanachama wa IGAD pamoja na Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Somalia, Sudan Kusini na Uganda.

Sudan imekuwa katika msukosuko tangu Aprili 15 wakati serikali inayoungwa mkono na wanajeshi na vikosi vya kijeshi vilipokabiliana kuhusu udhibiti huku nchi hiyo ikijiandaa kurejea kwa demokrasia ya kiraia.

TRT Afrika