Baadhi ya waandamanaji nje ya Jengo la KICC wakiandamana juu ya uchafuzi wa mazingira na uharibifu wa tabia nchi | Picha:  TRT Afrika

Wakati huo huo, baadhi waandamana katika mitaa ya Nairobi, wakiwa na mabango yenye ujumbe. Baadhi ya mabango hayo yanasema,

“Hasara na uharibifu,”

“Hakuna nishati ya kisukuku”

Huku nyingine zikisoma “Sema hapana kwa Uchafuzi,”

“Punguza maongezi zaidi kuhusu hatua za hali ya hewa”.

Wakati mkutano huo ukianza, baadhi ya waandamanaji wanaonekana katika mitaa ya jiji laNairobi, wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe tofauti. Picha: TRT Afrika

Haya yote na mengine yanawakilisha matarajio ya wananchi.

Huu ni Mkutano wa kwanza wa mabadiliko ya tabia nchi unaohudhuriwa na marais barani Afrika.

"Lazima tuone katika ukuaji wa kijani sio tu umuhimu wa hali ya hewa lakini pia chemchemi ya fursa za kiuchumi za mabilioni ya dola ambazo bara na Ulimwengu unatazamiwa kuzitumia," Rais William Ruto amesema.

Vijana wanataka ushirikishwaji zaidi katika utawala wa hali ya hewa, kwa matakwa kutoka kwa viongozi kutambua kukuza na kuwekeza katika mkutano wa vijana kama njia kuu ya maamuzi ya vijana.

Pia wameiomba serikali kuunda "kazi za kijani" kwa ajili ya vijana.

Huu ni Mkutano wa kwanza wa mabadiliko ya tabia nchi unaohudhuriwa na marais barani Afrika.

Vijana nao wanataka ushirikishwaji zaidi katika utawala wa hali ya hewa, na viongozi kutambua kukuza na kuwekeza katika mkutano wa vijana kama njia kuu ya maamuzi ya vijana.

Pia wameiomba serikali kutengeza fursa za ajira zinazotokana na mapambano ya tabia nchi.

Mabadiliko ya hali ya hewa ni ya kweli

"Lazima tuhakikishe kuwa fedha za hali ya hewa zinapatikana zaidi, zinapatikana kwa urahisi na zinaweza kupatikana kwa nchi zote zinazoendelea zikiwemo zile za Afrika," Rais Ruto ameongeza kusema.

Hata hivyo, mamilioni wanahisi mabadiliko ya hali ya hewa yanahitaji vitendo zaidi kuliko maneno.

Katika sehemu za Kenya, Somalia, Ethiopia na Sudan Kusini, wakaazi wamehisi na kuguswa na athari za kiangazi.

Tafiti zinaonyesha, katika sehemu za nchi ya Kenya, Somalia, Ethiopia na Sudan Kusini, wakaazi wanahisi kuguswa zaidi na athari za kiangazi.

"Zaidi ya watu milioni 31 katika nchi hizo nne wanakabiliwa na janga la njaa kali kwa sababu ya ukame na mafuriko ya miaka miwili," hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya Oxfam International.

"Ukame wa muda mrefu na mvua zisizokuwa na uhakika zimeua karibu wanyama milioni 13 na kuharibu mamia ya maelfu ya hekta za mazao na kuacha mamilioni bila mapato au chakula," inaongeza ripoti.

Vijana nao wanataka ushirikishwaji zaidi katika utawala wa hali ya hewa, na viongozi kutambua kukuza na kuwekeza katika mkutano wa vijana kama njia kuu ya maamuzi ya vijana.

Sehemu nyingine za bara hilo zinakabiliwa na athari za vimbunga, mafuriko na matetemeko ya ardhi.

Azimio la Nairobi

Je, mkutano huu wa kilele utakuwa tofauti kiasi gani na mikutano mengine iliyowahi kufanyika?

Vijana nao wanataka ushirikishwaji zaidi katika utawala wa hali ya hewa, na viongozi kutambua kukuza na kuwekeza katika mkutano wa vijana kama njia kuu ya maamuzi ya vijana.

Ajenda inabainisha maeneo makuu sita ya majadiliano kuhusu fedha za hali ya hewa, kukabiliana na ukuaji wa kijani, kukabiliana na hali ya hewa na ustahimilivu, hasara na uharibifu, vikundi vinavyoathiriwa na hali ya hewa, na uvumbuzi wa utafiti na teknolojia.

Kulingana na Tume ya Kiuchumi ya Umoja wa Mataifa kwa Afrika, ifikapo mwaka 2030, makadirio yanaonyesha kuwa Afrika inaweza kutumia asilimia 5 ya Pato la Taifa kwa mwaka kukabiliana na msukosuko wa hali ya hewa.

Wataalam wa masuala ya tabia nchi wanakadiria kuwa, Afrika itahitaji kati ya dola za Marekani bilioni 65 hadi 86.5 kwa mwaka kwa ajili ya kukabiliana na hali hiyo pekee hadi ifikapo mwaka 2030. Hivi sasa, bara hilo linapokea ufadhili wa kukabiliana na hali ya hewa wa kiasi cha dola bilioni 11.4 tu kwa mwaka.

Vijana nao wanataka ushirikishwaji zaidi katika utawala wa hali ya hewa, na viongozi kutambua kukuza na kuwekeza katika mkutano wa vijana kama njia kuu ya maamuzi ya vijana.

Wakati viongozi wa kisiasa na wataalamu wakipanga kujadili utata huu na mengine kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, mamilioni ya wakazi wa bara la Afrika wana wasiwasi kuhusu jinsi ya kulisha familia zao kutokana na athari za mabadiliko hayo.

TRT Afrika