Mashindano ya safari Rally yamefikia kilele huku Mkenya Carl Tundo akimaliza wa 12 kwa jumla  /Picha: WRC 

Sébastien Ogier alikaidi agizo la dereva-mwenza Kalle Rovanperä kutimiza ndoto yake ya 1-2-3-4 kwa Toyota Gazoo Racing katika siku ya mwisho ya kuvutia katika Safari Rally Kenya.

Mshindi wa mashindano haya ya kimataifa mwaka jana, 2022 alikuwa Kalle Rovanpera.

Kenya Safari Rally zimefikia kilele Jumapili 25 katika mji wa Naivasha Kenya. Picha WRC

Rais wa Kenya William Ruto alimtunukia Ogier na dereva mwenza Vincent Landais vikombe vya ushindi mjini Naivasha.

Kutoka 22 hadi 25 Juni mashindano yalikuwa ya kusisimua kwa wengi waliojitokeza kutazama.

Mashindano ya kimataifa ya magari Kenya 2023 / Picha AFP

Mashabiki walimiminika kutoka nchini Kenya na wengine kutoka nchi za kigeni

Mashindano ya kimataifa ya magari Kenya 2023 / Picha AFP

Kulikuwa na timu 20 kutoka nchi tofauti , Kenya iliwakilishwa na timu moja

Mashindano ya kimataifa ya magari Kenya 2023 / Picha Yasuyoshi CHIBA / AFP

Ilikuwa pia fursa ya Kenya kujenga utalii , kwani mashindano hayo ya magari yalipita katika mbuga ya wanyama.

TRT Afrika