Macky Sall anatarajiwa kujiuzulu kama rais wa Senegal mapema Aprili 2024. / Picha: Macky Sall

Rais anayemaliza muda wake wa Senegal Macky Sall amewaonya wagombea urais dhidi ya kutoa madai ya ushindi kabla ya wakati.

Si juu ya mgombea, wala kambi (ya kisiasa) kutangaza ushindi au matokeo," Sall alisema baada ya kupiga kura na mkewe katika mji wa magharibi wa kati wa Fatick siku ya Jumapili.

"Ni vituo vya kupigia kura ndivyo vitazungumza," Sall, ambaye hatagombea tena uchaguzi huo, aliongeza.

Wagombea 17 wa urais wanatafuta kumrithi Sall kama rais wa Senegal.

Zaidi ya raia milioni 7 wa Senegal walijiandikisha kama wapiga kura katika uchaguzi wa 2024, ambao ulicheleweshwa kwa utata kwa mwezi mmoja.

Mapema Februari, Sall alitangaza kwamba anaahirisha kwa muda usiojulikana uchaguzi wa urais wa Februari 25, lakini Baraza la Katiba la nchi hiyo lilimuamuru kufanya uchaguzi huo kabla ya kuondoka madarakani Aprili 2.

TRT Afrika