Makubaliano hayo yanaashiria dhamira ya kushiriki katika shughuli za pamoja zitakazochangia maendeleo na matumizi ya hifadhi ya petroli na gesi asilia ya Somalia. /Picha: Wizara ya Nishati na Maliasili ya Türkiye

Uturuki na Somalia zimetia saini mkataba wa uelewa kati ya serikali hadi serikali ili kuimarisha ushirikiano katika utafutaji wa mafuta na gesi asilia katika vitalu vya ndani na nje ya nchi ya Somalia.

Mkataba huo ulithibitishwa mbele ya Waziri wa Nishati na Maliasili ya Uturuki, Alparslan Bayraktar, na Waziri wa Somalia wa Mafuta na Madini, Abdirizak Omar Mohamed.

Chini ya makubaliano haya, juhudi za pamoja zitachukuliwa kuhakikisha rasilimali za Somalia zinatumiwa kwa manufaa ya watu wake, waziri wa Kituruki alisisitiza siku ya Alhamisi katika mtandao wa X.

Makubaliano hayo yanaashiria ahadi ya kushiriki katika shughuli za pamoja ambazo zitachangia katika kukuza na kutumia akiba ya mafuta na gesi asilia ya Somalia.

Hatua hii ya kimkakati ni sehemu ya lengo pana la Uturuki la kuimarisha uwepo wake katika Pembe ya Afrika kupitia ushirikiano mpya wa nishati, kukuza manufaa na ushirikiano katika eneo hilo, Bayraktar aliongeza.

Mkataba Muhimu

Makubaliano ya utafutaji mafuta na gesi asilia yalifikiwa wiki mbili baada ya bunge la Somalia kupitisha makubaliano ya ushirikiano wa ulinzi na uchumi wa pande mbili, makubaliano ya miaka 10 yanayoruhusu Uturuki kulinda bahari ya Somalia.

Mkataba huo sio tu inahusu kulinda maji ya Somalia bali pia inaandaa jukwaa la kuanzishwa kwa jeshi la wanamaji ili kulinda taifa la Pembe ya Afrika.

Mahusiano kati ya Uturuki na Somalia yamekuwa moja ya sifa kuu za sera ya nje ya Kituruki kuelekea Afrika.

Mwaka 2011, waziri mkuu wa wakati huo - sasa Rais Recep Tayyip Erdogan alikuwa kiongozi wa kwanza asiye wa Afrika kutembelea Somalia baada ya miongo miwili.

Tangu wakati huo, amezuru nchi hiyo mara kadhaa na kuwa mwenyeji wa wenzake wa Somalia nchini Uturuki mara kadhaa.

TRT World