Ndege ya shirika la ndege la Uturuki iliyokuwa na raia 142 wa Uturuki ilitua katika uwanja wa ndege wa Istanbul. / Picha: AA

Raia wa Uturuki na familia zao waliohamishwa kutoka Gaza kutokana na mashambulizi yanayoendelea Israel wamewasili Istanbul kupitia Misri.

Ndege ya shirika la ndege la Uturuki iliyokuwa na raia 142 wa Uturuki waliokuwa wamevuka mpaka na kuingia Misri kutoka kwenye kivuko cha mpaka cha Rafah ilitua katika uwanja wa ndege wa Istanbul mapema Jumatatu baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Cairo.

Wawakilishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki na maafisa kutoka Mamlaka ya Kudhibiti Maafa na Dharura ya Uturuki (AFAD) waliwakaribisha katika uwanja wa ndege.

Baadhi ya wanafamilia waliopokea waliohamishwa mjini Istanbul walishindwa kuzuia machozi yao.

Uturuki hapo awali alihamisha kundi la raia 42 wa Uturuki kutoka Gaza mnamo Novemba 19.

Jeshi la Israel lilianza tena kushambulia kwa mabomu Gaza mapema Ijumaa baada ya kutangaza kumalizika kwa mapatano ya wiki moja na kundi la muqawama la Palestina, Hamas.

Zaidi ya Wapalestina 15,500, wengi wao wakiwa watoto na wanawake, wameuawa katika mashambulizi ya Israel tangu Oktoba 7 kufuatia shambulio la kuvuka mpaka la Hamas.

TRT World