Watu walioshuhudia wameripoti kuwa wanajeshi wa Israel walifyatua risasi za moto dhidi ya kundi la Wapalestina waliokuwa wakishiriki maandamano ya kulaani makazi haramu kwenye Mlima Sbeih huko Beita, kusini mwa Nablus.

Uturuki imeelezea kusikitishwa kwake na kifo cha Aysenur Ezgi Eygi, raia wa Uturuki aliyeuawa na wanajeshi wa Israel huko Nablus, eneo linalokaliwa kwa mabavu la Ukingo wa Magharibi.

Katika taarifa yake, Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki ilitoa salamu za rambirambi kwa familia ya Eygi na kumtakia huruma ya Mungu.

Wizara ililaani "mauaji yaliyofanywa na Serikali ya Netanyahu."

"Israel inajaribu kuwatisha kila mtu anayekuja kusaidia Wapalestina na kupigana kwa amani dhidi ya mauaji ya halaiki. Sera hii ya ghasia haitaleta matokeo," wizara hiyo ilisema.

Taarifa hiyo ilionya zaidi kwamba "mamlaka za Israel zinazohusika na uhalifu dhidi ya ubinadamu, pamoja na wafuasi wao bila masharti, watawajibishwa mbele ya mahakama za kimataifa."

Kupinga makaazi haramu ya Israel

Mwanaharakati wa Kituruki mwenye asili ya Marekani aliuawa kwa kupigwa risasi na wanajeshi wa Israel siku ya Ijumaa wakati wa maandamano dhidi ya makazi haramu ya Waisraeli katika mji wa Beita katika wilaya ya Nablus katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.

Fouad Nafaa, mkurugenzi wa Hospitali ya Rafidia, alisema kuwa Aysenur Ezgi Eygi, ambaye ana uraia wa nchi mbili za Uturuki na Marekani, alifika hospitalini akiwa na jeraha la risasi kichwani.

Eygi, ambaye alizaliwa katika jiji la Uturuki la Antalya mwaka wa 1998, alifariki kutokana na majeraha licha ya majaribio ya timu za madaktari kutaka kumuokoa, kulingana na Nafaa.

Watu walioshuhudia wameripoti kuwa wanajeshi wa Israel walifyatua risasi za moto dhidi ya kundi la Wapalestina waliokuwa wakishiriki maandamano ya kulaani makazi haramu kwenye Mlima Sbeih huko Beita, kusini mwa Nablus.

Wakaazi wa Beita hufanya maandamano ya kila wiki baada ya sala ya Ijumaa kupinga makazi haramu ya Israel ya Avitar, ambayo yameanzishwa kwenye kilele cha Mlima Sbeih. Jamii inadai kuondolewa kwa makazi hayo haramu, ambayo wanayaona kama ukiukaji wa haki zao za ardhi.

TRT World