Uturuki imezindua "Operation Claw-Lock" mnamo Aprili 2022 kulisaka kundi la kigaidi la PKK kutoka mafichoni katika maeneo ya  kaskazini mwa Iraq, Metina, Zap na Avasin-Basyan karibu na mpaka wa Uturuki.​ ​​​​​​/Picha: AA

Vikosi vya usalama vya Uturuki vimewakata makali magaidi sita wa PKK kaskazini mwa Iraq, Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa ya nchi hiyo imesema.

"Jeshi letu la kishujaa la Uturuki limewakata makali magaidi sita wa PKK katika eneo la Operesheni ya Claw-Lock kaskazini mwa Iraq," Wizara hiyo ilisema Jumanne.

Wizara hiyo iliongeza kuwa shughuli za Uturuki za kukabiliana na ugaidi zitaendelea kwa dhamira na bila usumbufu.

Mamlaka ya Uturuki hutumia neno "kuwakata makali" ikimaanisha magaidi wanaohusika walijisalimisha au waliuawa au kukamatwa.

Katika kampeni yake ya takriban miaka 40 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na EU - imehusika na vifo vya zaidi ya watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake, watoto na watoto wachanga.

Uturuki ilizindua Operesheni Claw-Lock mwezi Aprili 2022 ili kuyavamia maficho ya kundi la kigaidi la PKK katika maeneo ya kaskazini mwa Iraq ya Metina, Zap na Avasin-Basyan karibu na mpaka wa Uturuki.

TRT World