"Mfumo wa kimataifa unaozingatia utawala wa sheria sio tu kwa baadhi, lakini kwa kila mtu. Ikiwa taasisi zinataka kudumisha uhalali wao, lazima ziwe pamoja na kila mtu," alisema Balozi Gulnur Aybet. / Picha: Jalada la AA

Gaza itajumuishwa katika ripoti za shughuli za siku zijazo za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kupitia mpango wa Uturuki.

Mwakilishi wa Kudumu wa Uturuki katika UNESCO, Balozi Gulnur Aybet, alisema Mkutano wa 219 wa Bodi ya Utendaji wa shirika hilo ulikuwa " wenye uzito na wenye tija" katika hotuba yake katika siku ya mwisho ya mkutano huo Jumatano.

Ingawa pande zote haziwezi kukubaliana juu ya kila kitu, lakini kwa kiwango fulani, zinaweza kufikia makubaliano juu ya baadhi ya mambo ambayo yanakubalika, mjumbe huyo alisisitiza.

Hii itaamua "tunaweza kuendeleza shirika hili kwa umbali gani," alisema.

Aybet alieleza kwamba “mfumo mzima wa Umoja wa Mataifa uliibuka kutoka kwenye majivu ya vita vyenye uharibifu katika kiwango cha kimataifa, ambapo ukatili ulifanywa, na kwa sababu hiyo, taasisi hizo zilianzishwa kwa lengo la ‘’kutotokea tena’’. Lakini vita na ukatili vinaendelea kutekelezwa licha ya kanuni za msingi za Umoja wa Mataifa.

Alionyesha wasiwasi kwamba wakati hakuna watoto wa kufundisha, waandishi wa habari kuripoti, au chochote kilichosalia kujenga upya, misheni ya taasisi hizi inapoteza umuhimu wake.

'Si kwa baadhi tu, bali kwa kila mtu'

Katika hotuba yake, mwakilishi wa Uturuki pia alisisitiza haja ya uwazi na ushirikishwaji wa nyaraka muhimu kwa wakati, akionyesha kwamba hii ingewezesha mijadala kuwa wenye tija.

"Hatupaswi kukwepa majadiliano. Mjadala ni mzuri; unatufanya tufahamu hisia za kila mmoja wetu, na hii ndiyo inayotufanya tuwe na nguvu kama UNESCO," alisema.

Wakati akiukaribisha plani ya Kazi ya UNESCO kwa Gaza, mjumbe huyo alionyesha kutoridhishwa na muundo wake wa uwasilishaji, akisisitiza kuwa ajenda zinapaswa kugawanywa na kujadiliwa na nchi wanachama kabla ya kikao kuanza, kuwezesha ujenzi wa maelewano.

Aybet aliwakumbusha wafanyakazi wenzake kwamba majukumu yao yanajumuisha kanuni za msingi za mfumo wa Umoja wa Mataifa, yakipita hata UNESCO, na kwamba katika wakati imani inapungua katika taasisi za kimataifa, ni wajibu wao kujenga upya uaminifu huu.

"Mfumo wa kimataifa unaozingatia utawala wa sheria sio kwa baadhi tu, bali kwa kila mtu. Ikiwa taasisi zinataka kudumisha uhalali wao, lazima ziwe pamoja na kila mtu," alisema, na kuzitaka taasisi zisiwe na hofu ya mabadiliko.

TRT World