Wananchi wameweka maua ya waridi meupe na mekundu kuwakumbuka walioathiriwa na mashambulizi ya Westgate/ Picha: AFP  / Photo: Reuters

Serikali ya Kenya imeahidi kuimarisha hatua za kiusalama dhidi ya wanamgambo wa Al Shabaab wakati ikiadhimisha miaka kumi tangu shambulio mbaya la maduka ya Westgate jijini Nairobi.

"Lengo letu ni kudumisha kiwango cha juu zaidi cha usalama katika mipaka yetu na operesheni za usalama kote nchini, na kuwazuia maadui kabla hajashambulia," Raymond Omollo, afisa mkuu wa wizara ya mambo ya ndani alisema Alhamisi katika taarifa yake ya maadhimisho ya miaka 10 ya mashambulizi hayo.

Kikundi cha wanamgambo wa Al Shabaab kilifanya mashambulizi kwa siku nne katika jumba la maduka la Westage / Picha:Reuters        

Maafisa wa serikali waliweka maua meupe na mekundu ya waridi nje ya lango kuu la maduka ya Westgate kwa heshima ya waathirika wa shambulio hilo.

Ni nini kilijiri Westgate 2013?

Wananchi kutoroka katika mashambulizi hayo vyovyote walivyoweza/ Picha: AFP 

Mnamo Septemba 21, 2013, watu wanne waliokuwa wamejifunika nyuso zao kwa bunduki walishambulia jumba la maduka maarufu Westgate jijini Nairobi.

Washambuliaji walianza kurusha mabomu na kuwafyatulia risasi watu waliokuwepo/ Picha:Reuters 

Watu hao walisimama kwenye lango kuu la Westgate Mall, wakiendesha gari aina ya Mitsubishi Lancer yenye namba za usajili KAS 575X.

Inaripotiwa walianza kurusha mabomu na kuwafyatulia watu risasi.

Baadhi waliweza kukimbia na wengine kuwasaidia wananchi wengine kutoroka kutoka kwenye eneo la tukio.

Kwa siku nne vikosi vya usalama vilipambana na magaidi hao/ Picha: AFP 

Washambuliaji walidai kuwa shambulio hilo lilikuwa la kulipiza kisasi kwa Kenya kutuma wanajeshi wake nchini Somalia mwaka 2011 na kupambana na wanamgambo wa al Shabaab.

Serikali ilidai kuwaua washambuliaji wote katika mlipuko/ Photo: AFP .

Kwa mujibu wa serikali ya Kenya, shambulio hilo lilisababisha vifo vya watu 67 huku ikidai kuwaua washambuliaji wote waliohusika.

TRT Afrika