Rais wa sasa Mokgweetsi Masisi atawania muhula wa pili na wa mwisho. / Picha: AFP

Umoja wa Afrika umetuma timu ya waangalizi nchini Botswana huku nchi hiyo ya Afrika kusini ikijitayarisha kufanya uchaguzi mkuu 30 Oktoba 2024.

Ujumbe huo utaongozwa na Goodluck Jonathan, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Shirikisho la Nigeria.

Ujumbe huo una waangalizi 30 wa muda mfupi , wakiwemo wataalam watatu ambao watakuwa daima.

Watafuatilizia uchaguzi kuanzia tarehe 22 Oktoba hadi 3 Novemba 2024.

Malengo ya ujumbe huo ni kutoa tathmini sahihi na isiyoegemea upande wowote na kuripoti ubora wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 30 nchini Botswana, ikiwa ni pamoja na kiwango ambacho uendeshaji wa chaguzi unakidhi viwango vya kikanda, bara na kimataifa kwa ajili ya kidemokrasia na uchaguzi.

Pia utatarajiwa kutoa mapendekezo ya kuboresha chaguzi zijazo kulingana na matokeo na kuonyesha mshikamano na uungaji mkono wa AU kuelekea uchaguzi na mchakato wa demokrasia wa Botswana ili kuhakikisha kwamba uchaguzi wa kidemokrasia, unaoaminika na wa amani unafanyika.

Rais wa sasa Mokgweetsi Masisi atawania muhula wa pili na wa mwisho baada ya chama chake tawala kuidhinisha azma yake ya kugombea kiti cha urais.

Rais anaruhusiwa mihula miwili madarakani, kwa mujibu wa katiba.

Tishio kuu la chama cha Masisisi BDP ni kutoka kwa muungano wa vyama, Umbrella for Democratic Change, au UDC, na Botswana Congress Party, ambayo imejitenga na muungano wa upinzani.

Tume Huru ya Uchaguzi nchini humo ilisajili tu 63% ya wapiga kura wanaostahiki licha ya kuwa wamelenga 80%.

Masisi alitangaza Oktoba 30 na 31 kama sikukuu za umma ili kuhamasisha wananchi kupiga kura.

TRT Afrika