Tanzania yafungua kiwanda cha kuzalisha umeme kwa maji katika eneo la Urithi wa Dunia

Tanzania yafungua kiwanda cha kuzalisha umeme kwa maji katika eneo la Urithi wa Dunia

Tanzania imewasha mtambo wa kwanza wa mfumo wa kuzalisha umeme kwa maji katika eneo la urithi wa UNESCO.
Tanzania imekuwa ikikabiliwa na tatizo la umeme, hali inayoendelea kuisababishia serikali maumivu makali ya kichwa. / Picha: AFP

Tanzania imewasha mtambo wa kwanza wa mfumo wa kuzalisha umeme kwa maji uliowekwa kwa uwezo wa kuzalisha umeme maradufu lakini jambo ambalo limepata upinzani mkali kutoka kwa wahifadhi kwa sababu ya kuwa katika eneo lililotengwa Umoja wa Mataifa la Urithi wa Dunia.

Doto Biteko, Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu, alisema alipotembelea Kiwanda cha kuzalisha umeme cha megawati 2,115 (MW) cha Julius Nyerere siku ya Jumapili kwamba turbine hiyo yenye uwezo wa MW 235 sasa inachangia umeme kwenye gridi ya taifa.

Alisema turbine hiyo itasaidia kupunguza mgao wa umeme wa miezi mingi, akiongeza kuwa mgao utaisha wakati turbine ya pili ya mfumo huo wa turbine tisa itakapokamilika kuunga gridi ya taifa mwezi ujao.

Kabla ya ujenzi wa mradi wa maji kuanza mwaka 2019, wahifadhi walitahadharisha kuwa kujenga bwawa kwenye mto mkubwa unaopita katika Pori la Akiba la Selous kunaweza kuathiri wanyamapori na makazi yao chini ya mto huo.

Juhudi za kuongeza usambazaji wa nishati

Hifadhi hiyo ni miongoni mwa maeneo makubwa zaidi ya hifadhi barani Afrika, ikihifadhi mojawapo ya wanyama wengi wakiwemo tembo, faru weusi na duma na aina kubwa ya makazi, kulingana na shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO.

Serikali iliendelea na mradi huo chini ya Rais wa zamani John Magufuli na mrithi wake Samia Suluhu Hassan unaona kuwa ni sehemu muhimu ya juhudi za kuongeza usambazaji wa umeme katika nchi ambayo chini ya nusu ya watu wanapata umeme.

Biteko alisema serikali itahakikisha miradi yote ya umeme wa maji inaheshimu uendelevu wa maji.

Kabla ya turbine ya kwanza ya Kiwanda cha Umeme wa Maji cha Julius Nyerere kuunganishwa kwenye gridi ya taifa, Tanzania ilikuwa na uwezo wa kuzalisha MW 1,601 huku gesi asilia ikichangia karibu theluthi mbili ya kiasi hicho.

TRT Afrika