Diamond  amesema hayuko tayari kuwa sehemu ya tuzo zenye kumbana msanii./Picha: Diamond Platnumz

Na Charles Mgbolu

Msanii mwenye tuzo nyingi nchini Tanzania ameweka wazi sababu za kutoshiriki kwenye tuzo za nchini mwake, na badala yake kushiriki zile za nje.

Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Diamond Platnumz alisema kutoshiriki kwenye tuzo hizo baada ya kuzitilia shaka.

‘’Unajua kwa nini sitaki kushirikishwa kwenye tuzo hizo? Kwa sababu zinaendeshwa bila haki," anasema.

Uwepo wake kwenye tuzo za ndani ya Tanzania ulionekana wazi mwaka 2023, aliposhinda tuzo ya Best African Act katika Tuzo za Muziki za MTV Europe.

Katika tuzo hizo, Diamond aliwashinda wasanii wengine wakali kama vile Burna Boy na Asake kutoka Nigeria na DJ Tyler ICU, wa Afrika Kusini.

Diamond amesema hayuko tayari kuwa sehemu ya tuzo zenye kumbana msanii.

‘’ Sihitaji huruma yoyote ili nishinde tuzo; ninapostahili, nipe, nisipostahili, basi uninyime. Mara nyingi, kamati ya maandalizi inataka kukubana. Katika umri wangu, siwezi kufanya hivyo,’’ alisema kwenye mkutano na wanahabari.

Diamond alishinda tuzo ya Best African Act katika tuzo za  MTV Europe mwaka 2023. /Picha: Platinum Facebook

Waandaaji wa tuzo nchini Tanzania wanakanusha madai ya kupendelea, wakisema tuzo hutolewa kwa wasanii ambao wametuma maombi na kuwasilisha kazi zao mbele ya majopo ya majaji.

Wakosoaji wa Diamond wamemtuhumu kuwa msanii anayepata shida kufuata sheria.

Mwaka jana, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), lilimfungia msanii huyo kufanya onesho lolote nchini Tanzania.

Uamuzi wa BASATA unafuatia hatua ya Diamond kutumbuiza wimbo uliopigwa marufuku nchini humo “Mwanza”, kwa kuwa na maudhui yasiyofaa kwa jamii.

Timu ya Diamond iliwaambia mashabiki kwenye mitandao ya kijamii wakati huo, kuwa juhudi zilikuwa zikifanywa kutatua marufuku hiyo na kurejesha maonyesho yote ya Diamond kwenye ratiba.

Diamond anasema malengo yake ya muziki yamepita zaidi ya kung’ang’ania tuzo za hapa nchini, huku macho yake yakiwa yanalenga kuutangaza muziki wa Tanzania duniani.

Pia aliwakosoa wapangaji wa maonyesho wa Nigeria, ambao anasema wanamdharau kama msanii.

“Wanaijeria wana tabia ya kukudharau, ingawa wanajua uwezo wako. Kwa hivyo onyesho linapotokea, nasema nataka kulipwa kiwango fulani. Ikiwa hutaki, sitaenda. Ndivyo ilivyo. Ufupi na wazi.’’

Mazungumzo kuhusu kutokuwepo kwa Diamond kwenye tuzo za ndani yameongezeka, haswa msimu wa tuzo za muziki wa 2024 ukikaribia kwa kasi.

Wawaniaji wa tuzo kuu za muziki barani kote wamepangwa kutangazwa kabla ya katikati ya mwaka, na mashabiki wa muziki nchini Tanzania wanatumai Diamond Platnumz ataingia kwenye orodha ya walioteuliwa, kupata tuzo zote ambazo anastahili.

TRT Afrika