Kwa picha : Mama Samia  aongoza Tanzania kuadhimisha miaka 60 ya Jeshi la Kujenga Taifa

Kwa picha : Mama Samia  aongoza Tanzania kuadhimisha miaka 60 ya Jeshi la Kujenga Taifa

Zaidi ya vijana 52000 wamesajiliwa mwaka huu kujiungana JKT
Vijana wote wanaofuzu kidato cha sita nchini Tanzania wanatakiwa kujiunga na JKT Picha : Ikulu Tanzania

Rais Samia ameongoza viongozi wengine, wakiwemo wa sasa na waliostaafu katika maadhimisho ya miaka 60 ya JKT katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

JKT, Pamoja na jukumu la malezi ya vijana wa taifa inakuza ubunifu na kutoa mchango katika kujenga taifa Picha Ikulu Tanzania 

Rais Samia ameelezea matamanio yake kuona jeshi la Kujenga Taifa likiiimarika na kuwa la kisasa katika utendakazi wake.

10 Julai 1963 Jeshi la Kujenga Taifa lilianzishwa rasmi kufuatia utekelezaji wa Azimio la Kikao cha Baraza la Mawaziri. Picha : Ikulu Tanzania

''Mafunzo ya JKT ni sehemu muhimu ya mchango wa amani tulionao Tanzania.'' Amesema waziri wa Ulinzi wa Tanzania, Innocent Lugha Bashungwa, wakati wa maadhimisho hayo ya miaka 60 ya JKT, jijini Dodoma.

Awali kujiunga na JKT ilikuwa jambo la kujitolea. Mwaka 1966 sheria hiyo ilifanyiwa marekebisho na kuanzisha utaratibu wa kujiunga JKT kwa mujibu wa Sheria. Picha : Ikuliu Tanzania 

''Vijana wanaopita JKT wanapaswa kubeba dhima ya uzalendo mioyoni mwao siyo katika midomo kwani jeshi linawafanya vijana kuwa wamoja na wenye kuithamini nchi yao katika kuonyesha uzalendo.'' amesema Mama Samia, alipokuwa akihutubia hafla hiyo.

JKT inashiriki katika mambo mbali mbali ya michezo na sanaa wanayoweza kuimarisha na kutumia talanta yao baada ya kuhitimu Picha : Ikulu Tanzania 

Waziri wa Ulinzi Innocent Bashugwa aliongeza kuwa, wizara yake itaendelea kushirikiana na wizara nyingine za kisekta kuboresha mafunzo stadi za kazi kwa vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa na kuwawezesha kuwapatia ujuzi na maarifa zaidi ya ilivyo sasa ili baada ya kuhitimu mafunzo ya JKT waweze kujitegemea.

Kikosi cah Jeshi la Kujenga Taifa kinapita mbele ya Mh Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya JKT mjini Dodoma Picha : Ikulu Tanzania 

“Katika miradi mikubwa mmefanya vizuri sana ikiwemo ujenzi wa Ikulu ya Chamwino, sisi Serikali tutaendelea kuwaunga mkono na ikibidi mpate mikopo ili kuongeza nguvu ya uzalishaji tuko tayari kuwadhamini,” amesema Rais Samia.

TRT Afrika