Nigeria, nchi yenye uchumi mkubwa zaidi barani Afrika, inakabiliwa na mzozo wa sarafu. /Picha: Wengine

Na Abdulwasiu Hassan

Kulingana na nadharia ya Robin Hood - ya kuchukua kutoka kwa matajiri, kuwapa maskini - itaonekana kuwa dawa ya haki kwa janga la kukosekana kwa usawa wa kiuchumi.

Mjadala huu ni kuhusi kiasi gani cha ushuru kinatosha kuleta mpatanisho wa amani amani na kile mwanasiasa wa Marekani Benjamin Franklin maarufu alisema, "Katika ulimwengu huu, hakuna kitu kinachoweza kusemwa kuwa hakika, isipokuwa kifo na kodi."

Mmoja wa wahisani tajiri zaidi duniani, mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates, alizua gumzo kwenye mitandao ya kijamii ya Nigeria hivi majuzi alipopendekeza kwamba taifa hilo la Afrika Magharibi lazima litozwe ushuru zaidi kwa raia wake.

"Ukusanyaji halisi wa ushuru nchini Nigeria uko chini sana," Gates alisema wakati wa ziara yake.

Gates si wa kwanza kuzungumzia suala la ukusanyaji wa chini wa kodi nchini Nigeria ikilinganishwa na Pato la Taifa.

Taasisi kama vile Shirika la Fedha la Kimataifa pia zimeashiria kile ambacho baadhi ya wataalam wanaamini kuwa ni hitilafu.

"Mwaka 2023, Nigeria ilikusanya asilimia 9.4 ya Pato la Taifa kupitia kodi. Hicho ni kiasi kidogo kabisa unaweza kuona duniani na barani Afrika," mkuu wa misheni ya Shirika la Fedha Duniani "IMF" nchini Nigeria, Axel Schimmelpfennig, alisema.

"Maana yake ni kwamba serikali ina rasilimali chache sana kwa matumizi ya kijamii na maendeleo katika afya, elimu, miundombinu, na kadhalika."

Pendekezo la kupunguza kodi

Kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta mwaka jana na kuelea kwa sarafu ya nchi hiyo, naira, kumesababisha mfumuko wa bei.

Mfumuko wa bei ulifikia rekodi ya juu baada ya sarafu ya Nigeria kuelea. /Photo: Reuters

Raia wengi wa Nigeria wamekuwa wakihangaika kutafuta riziki.

Mwenyekiti wa kamati ya rais ya sera ya fedha na marekebisho ya ushuru, Taiwo Oyedele, alisema hivi majuzi kuwa jopo hilo lilipendekeza kwa serikali kupunguza kodi ya 'VAT' hadi sifuri kwa chakula, afya, elimu, kodi, usafiri na biashara ndogo ndogo.

"Moja ya mambo tuliyogundua ni kwamba ni watu walioajiriwa ndio wengi nchini Nigeria ambao wamekuwa wakilipa kodi," alisema.

“Hivyo, ni wakati wao wa kupumzika maana yake ni lazima tuangalie upya mfumo wa kuwaondolea mzigo sehemu hatarishi wakiwemo wafanyabiashara wadogo, watu wa tabaka la kati na matajiri wana uwezo pia wa kulipa kodi, wakichangia ukusanywaji wa kodi kodi."

Kamati ya mageuzi ya kodi nchini Nigeria inataka VAT kwa mahitaji ya msingi kusitishwa. /Picha: Reuters

Oyedele alieleza kuwa kamati hiyo imetayarisha seti ya mabadiliko yaliyopendekezwa ambayo yanaweza kuimarisha upya fedha za nchi.

Rais Bola Tinubu hana budi kupata mapendekezo yaliyopitishwa na Bunge ili haya yawe sheria.

Kupungua kwa watu wa tabaka la kati

Sio kila mtu ana matumaini kama Oyedele kuhusu uwezekano wa kutoza ushuru ili kuziba pengo la mapato nchini.

Dk Usman Bello wa idara ya uchumi katika Chuo Kikuu cha Ahmadu Bello, Zaria, ni mmoja wao.

Anaamini kuwatoza ushuru watu wa tabaka la kati na matajiri kwa mapato ya juu una changamoto za kiutendaji.

"Lazima uelewe kwamba huwezi kutoza uchumi ambao tayari unakua polepole. Kupendekeza kwamba kodi zaidi inaweza kutozwa kwa mapato ya juu kutadhoofisha uchumi hadi kufikia hatua ya kushindwa kuvumilika," Dk Bello anaiambia TRT Afrika.

Anabainisha kuwa Wanigeria wengi wanaohamia kwenda kutafuta maisha mazuri ni watu wa tabaka la kati.

"Kutoza ushuru kwa watu hao hao wa tabaka la kati kutachochea zaidi uhamaji. Kwa hiyo, hakuna namna serikali inaweza kuendesha sera huria ambazo zinarudisha nyuma nyuma sana, ambapo unaanza kufikiri kwamba kodi kubwa ndiyo chaguo bora zaidi la kupata mapato ya serikali."

Pengo kwenye ukusanyaji wa ushuru

Mojawapo ya masuala muhimu kuhusu ushuru nchini Nigeria ni kwamba watu wengi nje ya sekta rasmi hawalipi kodi.

Bei za vyakula zimeongezeka hadi kiwango cha juu zaidi katika miongo kadhaa. /Picha: Reuters

Wakati wakosoaji wanalalamika kukosekana kwa utamaduni wa ukusanyaji kodi miongoni mwa Wanigeria wengi, wachambuzi wanasema uwajibikaji ndani ya tabaka la kisiasa huja kwanza.

Moja ya kanuni za kwanza za ushuru ni uwazi. Pili, ni kwa mlipa ushuru kujua kuwa pesa zake zinatumika kufadhili matumizi kwa faida kubwa ya umma, "anasema Dk Bello.

Ridwan Salisu Imam, ambaye anajipatia riziki kwa kuuza nafaka huko Kano, ni miongoni mwa wale ambao wangependa baadhi ya maswali kujibiwa kabla ya kulipa kodi kwa hiari.

"Nina haki ya kujua kama pesa ninazolipa kama ushuru zinatumika ipasavyo. Kila kitu kinarudi nyuma, huku viongozi wa serikali wakijenga au kununua nyumba za kifahari na kuwapeleka watoto shule nje ya nchi. Mfumo wetu wa elimu unaingia kwenye machafuko," inaiambia TRT Afrika.

"Makampuni makubwa na taasisi za fedha kama benki na makampuni ya kimataifa yanapaswa kutozwa ushuru zaidi."

Kutoza ushuru kwa matajiri

Kuna dhana kwamba kutoza kodi kwa matajiri zaidi kutakuwa na athari ndogo katika mapato ya serikali kwani matajiri wa Nigeria wanajumuisha sehemu ndogo ya watu milioni 218 nchini humo.

Uchumi wa Nigeria kwa kiasi kikubwa sio rasmi. Picha: Wengine

Nadharia nyingine ni kwamba Nigeria inaweza kufaidika kutokana na kutoza ushuru bidhaa na huduma za anasa. Moja ya hayo ni ndege za kibinafsi. Mamlaka ya forodha ilikemea huduma za kukodisha ndege hivi karibuni kwa sababu hawana nyaraka zinazofaa kwa ndege zao.

Serikali pia ilikuwa imetishia kuwabana wanaoshughulikia ndege za kibinafsi mnamo 2021, lakini haikufanikiwa sana.

TRT Afrika