Madaktari wamekuwa katika mgomo tangu Machi 13, 2024 / Picha: Reuters

Muungano wa Kitaifa wa Maafisa wa Maabara ya Matibabu nchini Kenya (KNUMLO) umetoa notisi ya mgomo wa siku saba kwa Wizara ya Afya kuzingatia matakwa yake.

Katibu Mkuu wa Muungano Pius Nyakundi amesema maafisa hao wa maabara walitoa uamuzi kwa serikali ya kitaifa na kaunti kuwathibitishia wanafunzi wanaofanya kazi katika Huduma ya Afya kwa Wote (UHC) na wafanyakazi wengine katika masharti ya Kudumu na Pensheni miongoni mwa masuala mengine.

“Tunazipa rasmi ngazi zote mbili za Serikali (Kitaifa na Serikali za Kaunti 47) notisi ya siku Saba (7) ya mgomo kwa sababu zifuatazo:- Kushindwa kwa Serikali kuunda Mkataba wa Utambuzi na Muungano licha ya kuwa imekidhi matakwa ya Sheria hata baada ya majaribio kadhaa ya kutaka suala hili litatuliwe kwa njia ya amani,” taarifa hiyo ilisema.

Kulingana na Muungano, Wizara imeshindwa kutekeleza makubaliano ya awali ambayo yalitakikana kutatua baadhi ya mahitaji ya KNUMLO.

"Kushindwa kufanyia kazi mambo yaliyotajwa hapo juu, mgomo huo utaanza Jumanne, Aprili 2, 2024,... na utaendelea hadi masuala yote yaliyomo yatakapotatuliwa kikamilifu."

"Serikali ianze mara moja kuwatambua Wataalamu wa Maabara ya Tiba kama sehemu muhimu ya mfumo wa Huduma ya Afya, kukomesha ubaguzi na kutengwa kwa wataalamu katika kufanya maamuzi na kuwaleta wasimamizi wote wa maabara kwenye mfumo wa usimamizi wa afya," wataalamu hao wamedai.

Umoja huo pia unaitaka Wizara hiyo kutekeleza ajira za Wataalamu 10,000 wa Maabara ya Tiba ili kukabiliana na upungufu uliokuwepo zaidi wakiitaka Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) kuwalipa wafanyakazi wake Posho ya Hatari ya Afya kwa Wanachama wa Shahada ambao hawajapata posho hiyo.

Tayari madaktari nchini wapo kwenye mgomo waliouanza Machi 13, 2024.

Madaktari hao wanaitaka serikali kuwatuma kazini wanafunzi wahudumu wa afya mara moja na kufuta malimbikizo ya mishahara ya madaktari kulingana na Makubaliano ya Pamoja ya 2017.

TRT Afrika