Afrika Magharibi imekuwa na ongezeko ya majaribio ya mapinduzi ya serikali/ Picha: AP

Mapinduzi ya serikali ni jaribio la kumuondoa madaraka kiongozi aliye madarakani au kutwaa madaraka.

Kati ya nchi 54 katika bara la Afrika, 45 zimekuwa na angalau jaribio moja la mapinduzi tangu 1950.

Ni nchi gani za Kiafrika zimepitia majaribio mengi ya mapinduzi?

Sudan imekuwa na mapinduzi mengi yaliyojaribiwa na kufanikiwa.

Tangu kupata uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo 1956, kumekuwa na jumla ya majaribio 17 ya mapinduzi ambapo sita kati yao yaliyofaulu mnamo 1958, 1969, 1985, 1989, 2019 na 2021.

Burundi imekumbwa na majaribio 11 (6 yamefaulu na 5 hayakufaulu) na Ghana majaribio 10 (5 yamefaulu na 5 yameshindwa).

Ni nchi gani hazijawahi kukumbana na aina yoyote ya mapinduzi ya kijeshi katika historia yao?

  • Botswana
  • Mauritius
  • Senegal
  • Cape Verde
  • Malawi
  • Eritrea
  • Namibia
  • Sudan Kusini
TRT Afrika