Guinea president escapes prison

Taarifa kutoka wizara ya haki na sheria ya Guinea imethibitisha kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Kapteni Moussa Dadis Camara alitoroka gerezani Jumamosi hii.

Ripoti zilisema milio ya risasi ilisikika kwa mara ya kwanza mwendo wa saa nne asubuhi kwa saa za huko (0400 GMT) ambapo usalama uliimarishwa katika mitaa ya Conakry na lango la kuingia Kaloum likazuiwa.

Katika taarifa, Charles Alphonse Wright, Waziri wa sheria na haki wa Guinea, alieleza kuwa ''ilikuwa saa 5 asubuhi ambapo watu wenye silaha walichukua udhibiti wa gereza kuua la Conakry. Walifanikiwa kuondoka na Kapteni Moussa Dadis Camara, pamoja na maafisa wengine waliokuwa wamefungwa pamoja naye kutoka utawala wake, Claude Pivi na Moussa Tiegboro Camara na Blaise Goumou,'' ilisema taarifa.

Kanali Thiegboro Camara, aliyetoroka pamoja nao, alipatikana na kukamatwa na kurejeshwa katika nyumba kuu ya Conakry. Mipaka yote imefungwa.''

Waziri wa sheria Wright, alielezea kukasirishwa na tukio hilo na aliahidi kwamba waliotoroka wangepatikana haraka sana.

''Tutawapata. Na lazima husika watajibu masuali kwa sababu tunashangaa jinsi watu wenye silaha wanaweza kuvunja ulinzi mkali gereza kuu, kwenda kuchukua wafungwa. Inaonekana ajabu, majukumu yatapatikana. Hakukuwa na ripoti za vifo wala majeruhi. Waliotoroka watatafutwa hadi eneo lao la mwisho,'' aliongeza.

Risasi nzito zinalia Conakry huku mji ukifungiwa

Rais huyo wa zamani wa Guinea alifungwa katika gereza kuu la Conakry, baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika au kuidhinisha matukio ya Septemba 28, 2009, wakati wanajeshi walipoua takriban watu 157 na kuwabaka wanawake 109 katika uwanja wa michezo ambapo maelfu ya wapinzani walikusanyika kugombea kwa mkuu wa junta wakati huo, Kapteni Moussa Dadis Camara, kulingana na tume ya kimataifa ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa.

TRT Afrika