Mkataba wa UAE-Ethiopia unaruhusu kubadilishana dirham ya Imarati na birr ya Ethiopia yenye thamani ya dirham bilioni 3 na birr bilioni 46. / Picha: Reuters

Ethiopia, inayokabiliwa na uhaba mkubwa wa fedha za kigeni, ilitia saini makubaliano ya kubadilishana sarafu na Umoja wa Falme za Kiarabu, taarifa ya pamoja ilifichuliwa Jumanne.

Makubaliano hayo, yaliyotiwa wino kati ya Benki ya Kitaifa ya Ethiopia (NBE) na Benki Kuu ya UAE (CBUAE), inaruhusu kubadilishana dirham ya Imarati na birr ya Ethiopia yenye thamani ya dirham bilioni 3 na birr bilioni 46.

"Mkataba wa kubadilishana sarafu baina ya nchi mbili na MoUs (mkataba wa maelewano) uliotiwa saini leo unaonyesha ushirikiano thabiti wa kiuchumi kati ya UAE na Ethiopia, hasa katika maeneo ya biashara na uwekezaji," alisema Gavana wa CBUAE Khaled Mohamed Balama.

Gavana wa NBE Mammo Mihretu alisisitiza alisisitiza jukumu muhimu la UAE katika uchumi wa Ethiopia. Alisema UAE ni "chanzo kikubwa cha uwekezaji wa kigeni na fedha za maendeleo."

Upungufu wa fedha za kigeni

Zaidi ya hayo, hati mbili zilitiwa saini ili kukuza matumizi ya fedha za ndani katika shughuli za mipakani na kuimarisha ujumuishaji wa mifumo ya malipo na teknolojia ya kifedha kati ya mataifa hayo mawili.

Ethiopia, ambayo ina akiba ya sasa ya dola bilioni 3.046, imekuwa ikikabiliwa na uhaba wa fedha za kigeni na mazungumzo na Shirika la Fedha la Kimataifa na Benki ya Dunia yamekwama.

Mazungumzo haya ni sehemu ya juhudi za Ethiopia kurekebisha deni lake na kupata ufadhili wa ziada ili kuleta utulivu wa uchumi wake.

IMF na Benki ya Dunia zimekuwa zikiitaka Ethiopia kutekeleza mageuzi ya kiuchumi na kuboresha usimamizi wa fedha ili kukabiliana na changamoto za kifedha za nchi hiyo.

TRT Afrika