Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, na mwenzake wa Marekani wajadili  yanayoendelea Gaza

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, na mwenzake wa Marekani wajadili  yanayoendelea Gaza

Hakan Fidan amemwambia Antony Blinken kuwa kulenga watu wa Gaza kwa pamoja haikubaliki, vyanzo vya kidiplomasia vimesema
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan / Picha: AA

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken wamejadili maendeleo ya hivi karibuni huko Gaza kwa njia ya simu, vyanzo vya kidiplomasia vilisema Jumapili.

Wanadiplomasia hao wawili wa juu walizungumza kuhusu kuzuia mzozo wa Gaza kuenea katika mkoa huo, na juhudi za kufanikisha kuachiliwa kwa mateka na uharaka wa kutenga njia salama itakayotumika kufikisha misaada ya kibinadamu pamoja na mchakato wa upanuzi wa NATO, vyanzo vilisema.

Fidan aliendelea kumwambia Blinken kwamba kulenga watu wa Gaza kwa pamoja hakukubaliki.

Israel imezidisha mashambulizi yake ya anga na ardhini huko Gaza kufuatia shambulio la kushtukiza la Hamas zaidi ya wiki tatu zilizopita ambapo mamlaka ya Israel inasema imewauwa takriban watu 1,400.

Takriban watu 9,500 wameuawa katika mashambulizi hayo, wakiwemo Wapalestina 8,005, wengi wao watoto 3,342, wanawake 2,062 na wazee 460, kulingana na Wizara ya Afya.

Zaidi ya Waisraeli 1,538 wameuawa tangu kuzuka kwa mgogoro wa Gaza mnamo Oktoba 7, Shirika la Habari la Umma KAN limesema.

Msemaji wa jeshi la Israeli Daniel Hagari alitangaza Jumamosi kwamba vikosi vya Israeli vilikuwa vinapanua shughuli zao na kuelezea kile walichokiita "awamu inayofuata ya vita vyetu dhidi Ya Hamas," ambayo ni pamoja na shughuli za ardhini.

Haya yanajiri huku wakazi milioni 2.3 wa Gaza wakikabiliwa na uhaba wa chakula, maji, mafuta na dawa kutokana na vikwazo vya Israeli katika eneo hilo.

TRT World