Mamlaka ya Uturuki yanatumia neno "kukata makali" kumaanisha kwamba magaidi husika walijisalimisha au waliuawa au kutekwa. / Picha: AA

Vikosi vya usalama vya Uturuki "vimewakata makali" magaidi 65 wa PKK/YPG kaskazini mwa Iraq na kaskazini mwa Syria katika kipindi cha wiki moja iliyopita, Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa ya nchi hiyo imesema.

"Magaidi sitini na watano walikatwa makali katika wiki iliyopita. Kwa hivyo, jumla ya magaidi walioangamizwa kaskazini mwa Iraq na Syria tangu Januari 1 imefikia 1,828," msemaji wa wizara na Afisa wa Jeshi la Majini Zeki Akturk alisema katika mkutano wa kila wiki wa waandishi wa habari katika mji mkuu Ankara siku ya Alhamisi.

Hasa, gaidi mmoja wa PKK kutoka kaskazini mwa Iraq alijisalimisha kwa kituo cha mpakani cha Uturuki huko Habur wiki iliyopita, Akturk aliongeza.

Mamlaka ya Uturuki yanatumia neno "kukata makali" kumaanisha kwamba magaidi husika walijisalimisha au waliuawa au kutekwa.

Akturk pia alisema watu 394, ikiwa ni pamoja na wanachama 15 wa makundi ya kigaidi, walikamatwa wakati wakijaribu kuvuka mpaka kinyume cha sheria katika wiki iliyopita, wakati wengine 1,370 walizuiwa kuvuka.

"Idadi ya watu waliokamatwa wakijaribu kuvuka mipaka yetu kinyume cha sheria tangu Januari 1, 2024, imeongezeka hadi 9,067, na idadi ya watu waliozuiwa kuvuka mpaka imefikia 72,082,” alisema.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na EU - imehusika na vifo vya karibu watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake, na watoto. Kundi la YPG ni tawi la PKK nchini Syria.

TRT World