Uturuki yafanya mashambulizi ya anga na kuharibu maficho ya PKK kaskazini mwa Iraq

Uturuki yafanya mashambulizi ya anga na kuharibu maficho ya PKK kaskazini mwa Iraq

Magaidi wengi "wamekatwa makali " kufuatia operesheni inayoendelea  maeneo mengi kaskazini mwa Iraq.
Picha AA

Ndege za kivita za Uturuki zilifanya mashambulizi ya anga katika maeneo ya PKK kaskazini mwa Iraq kwa mujibu wa haki ya Umoja wa Mataifa ya kujilinda, Wizara ya Ulinzi ya Uturuki imetangaza.

Operesheni ya kupambana na ugaidi ya Jumapili jioni ilikuja baada ya magaidi wawili kushambulia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uturuki katika mji mkuu wa taifa hilo, Ankara, saa chache kabla ya hotuba ya Rais Recep Tayyip Erdogan bungeni.

"Magaidi wengi walikatwa makali kwa kutumia kiwango cha juu zaidi cha risasi za ndani na za kitaifa katika operesheni zilizofanywa," Wizara ya Ulinzi ilisema katika taarifa.

Wakati wa operesheni hiyo, takriban maficho 20 ya PKK ikiwemo mapango, malazi na bohari katika maeneo ya Metina, Hakurk, Kandil na Gara kaskazini mwa Iraq ililengwa, kulingana na taarifa.

Kampeni hiyo ya anga ilifanywa ili "kuondoa mashambulio ya kigaidi dhidi ya watu wetu na vikosi vya usalama kutoka kaskazini mwa Iraqi kwa kuwatenganisha PKK/KCK na magaidi wengine na kuhakikisha usalama wa mpaka wetu," wizara ilisema.

Shambulio la kigaidi

Mapema siku ya Jumapili, mshambuliaji wa kujitoa mhanga alilipua kifaa karibu na lango la Idara ya Usalama ya Wizara ya Mambo ya Ndani, na kuwajeruhi maafisa wawili wa polisi.

Mshambuliaji wa pili aliuawa katika majibizano ya risasi na polisi, waziri wa mambo ya ndani alisema.

Maafisa wa polisi waliojeruhiwa bado wanatibiwa, na majeraha yao sio hatari kwa maisha, kulingana na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya. Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Ankara ilianzisha uchunguzi kuhusu shambulio hilo la kigaidi.

TRT World