Simu hiyo pia ilishughulikia uhusiano wa nchi mbili kati ya Uturuki na Uhispania pamoja na maswala ya kikanda na kimataifa. / Picha: Jalada la AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Waziri Mkuu wa Hispania Pedro Sanchez wamezungumza kwa njia ya simu na kujadili mashambulizi yasiyoisha ya Israel kule Gaza.

Kulingana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki, Erdogan alimwambia Sanchez Jumatatu: "Mauaji ya Israel dhidi ya Palestina lazima yasitishwe haraka iwezekanavyo na Israel ilazimishwe kuzingatia sheria za kimataifa."

Akikaribisha uamuzi wa Hispania wa kutambua Palestina kama taifa, rais wa Uturuki pia alielezea imani yake kuwa hatua hii itaimarisha uanzishwaji wa amani na haki katika eneo hilo na juhudi za suluhisho la mataifa mawili.

Simu hiyo pia ilizungumzia mahusiano ya pande mbili kati ya Uturuki na Hispania pamoja na masuala ya kanda na kimataifa.

Katika taarifa kwenye X, Sanchez alisema yeye na Erdogan walijadili kutambuliwa kwa Taifa la Palestina na Hispania na umuhimu wa kufikia "makubaliano ya amani ambayo yatamaliza kabisa vurugu."

"Tumechambua na Rais Erdogan kuhusu Mkutano ujao wa Kiserikali ambao nchi zote mbili zitafanya Madrid mwezi Juni. Mfano mwingine wa kuimarisha mahusiano bora kati ya Hispania na Uturuki," Sanchez aliongeza.

Israel imeua zaidi ya Wapalestina 36,000 huko Gaza tangu shambulio la mpakani na Hamas mnamo Oktoba 7 mwaka jana, ambalo liliua takriban watu 1,200.

Mabomu hayo yamegeuza sehemu kubwa ya eneo la watu milioni 2.3 kuwa magofu, na kuwaacha raia wengi bila makazi na katika hatari ya njaa.

TRT World