"Tutaendelea kuunganisha Karne ya Uturuki na baraza letu jipya la mawaziri," anasema Erdogan katika hafla ya kuapishwa kwake. / Picha: AA

Recep Tayyip Erdogan amezindua Baraza jipya la Mawaziri la Türkiye katika Ikulu ya Rais ya Cankaya katika mji mkuu Ankara baada ya kuapishwa kama rais bungeni.

Erdogan siku ya Jumamosi alimtangaza naibu waziri mkuu wa zamani Cevdet Yilmaz kuwa Makamu wake wa Rais.

Wajumbe wa Baraza jipya la Mawaziri ni kama ifuatavyo:

Waziri wa Sheria: Yilmaz Tunc

Waziri wa Huduma za Familia na Jamii: Mahinur Ozdemir Goktas

Waziri wa Kazi na Usalama wa Jamii: Vedat Isikhan

Waziri wa Mazingira, Ukuaji wa Miji na Mabadiliko ya Tabianchi: Mehmet Ozhaseki

Waziri wa Mambo ya Nje: Hakan Fidan

Waziri wa Nishati na Maliasili: Alparslan Bayraktar

Waziri wa Vijana na Michezo: Osman Askin Bak

Waziri wa Hazina na Fedha: Mehmet Simsek

Waziri wa Mambo ya Ndani: Ali Yerlikaya

Waziri wa Utamaduni na Utalii: Mehmet Nuri Ersoy

Waziri wa Elimu Kitaifa: Yusuf Tekin

Waziri wa Ulinzi Kitaifa: Yasar Guler

Waziri wa Afya: Fahrettin Koca

Waziri wa Viwanda na Teknolojia: Mehmet Fatih Kacır

Waziri wa Kilimo na Misitu: Ibrahim Yumakli

Waziri wa Biashara: Omer Bolat

Waziri wa Uchukuzi na Miundombinu: Abdulkadir Uraloglu

'Karne ya Uturuki' inaanza Akizungumza katika hafla ya kuapishwa kwake, pamoja na mahudhurio ya maafisa wa ngazi za juu kutoka nchi 81, Erdogan alisema mkutano wa kwanza wa baraza la mawaziri chini ya uenyekiti wake utafanyika Jumanne.

"Tutaendelea kuunganisha Karne ya Uturuki na baraza letu jipya la mawaziri," alisema.

Erdogan aliapa kufanya kazi kwa kujitolea katika miaka mitano ijayo "kulinda utukufu na heshima ya Jamhuri ya Uturuki, kukuza sifa yake na kulitukuza jina lake duniani kwa miaka mitano."

Kuapishwa kwake kulihudhuriwa na wakuu 50 wa nchi, mawaziri wakuu 13, mabunge, maofisa wa ngazi ya mawaziri na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, yakiwemo NATO, Jumuiya ya Nchi za Turkic, na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu.

Miongoni mwa waliohudhuria ni Rais wa Azerbaijan Ilham Aliyev, Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini Ersin Tatar, Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif na Waziri Mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan.

Hapo awali, Erdogan alikula kiapo cha kuhudumu katika Bunge la Uturuki kwa muhula wake mpya wa urais wa miaka mitano.

Uturuki ilipiga kura mnamo Mei 28 kwa duru ya pili ya urais baada ya kukosa mgombeaji aliyepata zaidi ya asilimia 50 ya kura zinazohitajika kwa ushindi wa moja kwa moja katika duru ya kwanza mnamo Mei 14.

Erdogan alishinda kinyang’anyiro hicho kwa kupata asilimia 52.18 ya kura, huku mgombea wa upinzani Kemal Kilicdaroglu akipata asilimia 47.82.

TRT World