Ninakumbuka kaka na dada zetu wa Bosnia ambao walichukuliwa kutoka kwetu na kushiriki kwa dhati uchungu wa familia zao na wapendwa waliopoteza maisha yao. /Picha: AA

Mke wa Rais wa Uturuki Emine Erdogan ametafakari juu ya mauaji ya halaiki ya Srebrenica katika kumbukumbu ya miaka 29, na kuyataja kama "sura ya aibu katika historia ya binadamu."

"Ninalaani tena mauaji ya halaiki ya Srebrenica, ambayo yaligeuza ardhi za Bosnia kuwa watumwa wa huzuni na machozi, mauaji hayo yaonyesha sura ya aibu katika historia ya mwanadamu, katika siku ya kumbukumbu ya miaka 29," alisema kwenye mtandao wa X.

"Ninakumbuka kaka na dada zetu wa Bosnia ambao walichukuliwa kutoka kwetu na kushiriki kwa dhati uchungu wa familia zao na wapendwa waliopoteza maisha yao."

Uturuki ilitangaza rasmi Julai 11 kama "Siku ya Kimataifa ya Kutafakari na Kukumbuka Mauaji ya Kimbari ya Srebrenica" kulingana na amri ya rais iliyochapishwa kwenye Gazeti Rasmi Jumatano.

Katika msimu wa masika 1993, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilitangaza Srebrenica "eneo salama." Hata hivyo, wanajeshi wa Serbia wakiongozwa na Jenerali Ratko Mladic, ambaye baadaye alipatikana na hatia ya uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya ubinadamu, na mauaji ya halaiki, waliteka eneo lililolindwa na Umoja wa Mataifa.

Wanajeshi wa Uholanzi waliohusika na kulinda watu katika eneo la Umoja wa Mataifa walishindwa kuchukua hatua wakati vikosi vya Waserbia vilikalia eneo hilo mnamo Julai 11, na kuua wanaume na wavulana 2,000 kwa siku moja.

Takriban Wabosnia 15,000 walikimbilia milima iliyowazunguka, lakini wanajeshi wa Serbia waliwashambulia, na kuua watu wengine 6,000.

Vikosi vya Waserbia viliruhusu wanawake na watoto kufikia maeneo yanayodhibitiwa na Bosnia lakini waliwaua angalau wanaume 8,372 wa Bosnia katika misitu, viwanda na maghala.

Wabosnia waliouawa walizikwa katika makaburi ya halaiki, huku miili ikigunduliwa katika maeneo 570 tofauti nchini kote, yakiwemo makaburi 77 ya halaiki.

Mnamo 2007, Mahakama ya Kimataifa ya Haki huko The Hague iliamua kwamba mauaji ya halaiki yalifanywa huko Srebrenica.

Juhudi za kuwatafuta wahanga waliotoweka wa mauaji ya kimbari zimeendelea, huku mabaki yaliyotambuliwa yakizikwa katika makaburi ya kumbukumbu ya Potocari katika siku ya kumbukumbu inayofanyika kila mwaka Julai 11.

Kufikia sasa, wahasiriwa 6,751 wamezikwa katika Makaburi ya Ukumbusho ya Potocari, na wahasiriwa 250 wamezikwa kwenye makaburi ya ndani kwa ombi la familia zao. Huku zaidi ya waathiriwa elfu moja hawajulikani walipo.

Mnamo Juni 8, 2021, majaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa waliidhinisha kifungo cha maisha kwa Mladic kwa mauaji ya halaiki, mateso, uhalifu dhidi ya ubinadamu, kuangamiza, na uhalifu mwingine wa kivita uliofanywa nchini Bosnia na Herzegovina.

Maadhimisho ya mwaka huu yatashuhudia wahasiriwa wengine 14 waliotambuliwa n kama waathiriwa wa mauaji wa halaiki wakiwa wamezikwa katika makaburi ya kumbukumbu ya Potocari.

TRT World