Kadi za utambulisho ghushi pamoja na kiasi kikubwa cha fedha na nyenzo za kidijitali pia zilinaswa wakati wa operesheni hiyo  / Picha: AA 

Zekeriye Cerit, anayejiita mkurugenzi wa Turkmenistan wa Shirika la Kigaidi la Fetullah (FETO), na gaidi mwingine mtoro wamekamatwa na mamlaka ya Uturuki Istanbul.

Baada ya kupewa taarifa kwamba magaidi hao watatoroka nje ya nchi, operesheni mbili tofauti zilifanywa na kitengo kikuu cha usalama na polisi wa kupambana na ugaidi wa Uturuki, kulingana na taarifa iliyopokelewa na Anadolu.

Wakati wa operesheni hiyo, Zekeriye Cerit, ambaye yuko kwenye orodha ya "wanaosakwa kwa ajili ya ugaidi " alikamatwa mjini Istanbul, kwa ajili ya utakatishaji wa fedha wa shirika hilo katika vyama vinavyomilikiwa na FETO na kwa kuwa mkurugenzi wa shirika la kigaidi nchini Turkmenistan.

Dola za Marekani $3,300 na €180 (takriban dola $197) pesa taslimu, vitambulisho ghushi, na idadi kubwa ya nyenzo za kidijitali pia zilinaswa wakati wa operesheni hiyo FETO iliandaa mapinduzi yaliyoshindwa ya Julai 15, 2016, mjini Uturuki, ambapo watu 251 waliuawa na 2,734 kujeruhiwa.

TRT Afrika na mashirika ya habari