Muungano wa Erdogan’s People’s Alliance umepata wingi wa kura bungeni, huku kinyang’anyiro cha urais kikielekea kwenye duru ya pili ya marudio Mei 28. / Picha: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameapa kushinda ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa marudio wa rais wa Mei 28. "Sasa ni wakati wa kutwaa taji la mafanikio tuliyopata tuliyopata Mei 14 kwa ushindi mkubwa," Erdogan alisema kwenye Twitter.

Mamilioni ya wapiga kura walijitokeza siku ya Jumapili kumchagua rais wa nchi hiyo na pamoja na wabunge 600. Muungano wa Erdogan wa People’s ulipata wingi wa kura bungeni, huku kinyang’anyiro cha urais kinaelekea kwa duru ya pili ya marudio Mei 28, ingawa Erdogan aliongoza katika awamu ya kwanza.

Erdogan na mshindani wake wa karibu Kemal Kilicdaroglu, kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Chama cha watu wa Kijamhuri (CHP) na mgombea mwenza wa Muungano wa vyama sita vya upinzani vya Muungano wa Kitaifa, watachuana katika raundi ya pili.

"Sisi ni muungano unaoweka utashi wa kitaifa na upendo wa kutumikia nchi, na taifa katikati ya siasa zake," Erdogan alisema.

Aliongeza kuwa wanaweza tu kulipa deni la shukrani kwa taifa kwa kufanya kazi kwa bidii zaidi.

"Uturuki inatarajia huduma kutoka kwetu, inatarajia matokeo. Taifa letu linatarajia kufikia malengo yake," alisema.

TRT Afrika