Rais wa Uturuki Erdogan ajibu maswali ya waandishi wa habari katika ndege yake akirejea kutoka Ugiriki. /Picha: Nyingine / Photo: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alijibu maswali ya waandishi wa habari katika safari yake ya kurejea kutoka Ugiriki kufuatia mkutano wa 5 wa Baraza la Ushirikiano wa Ngazi ya Juu la Uturuki na Ugiriki, yaani Türkiye-Greece High Level Cooperation Council.

Rais Erdogan alisema siku ya Alhamisi, anaamini enzi mpya itaanza kwa uhusiano wa Uturuki na Ugiriki baada ya ziara yake huko Athens, ambayo ilikuwa nzuri sana.

Ameongeza kuwa, nchi hizo mbili zilijadili uhusiano wa pande mbili, ikiwa ni pamoja na biashara na utalii, bahari ya Mediterania na uwezekano wa ushirikiano wa nishati, na hali ya Gaza ya Palestina.

Katika ziara yake hiyo rais wa Uturuki alikutana na rais wa Ugiriki Katerina Sakellaropoulou na waziri mkuu wa Ugiriki Kyriakos Mitsotakis mjini Atina.

Kuhusu mzozo wa nishati katika eneo la Mediterania ya Mashariki, Rais Erdogan alisisitiza uwezekano wa kushirikisha nchi za kikanda kwa ushirikishwaji na haki.

Pia alipendekeza kupanua ushirikiano kwa kujumuisha nishati ya nyuklia, kuongeza kiwango kuelekea usafirishaji wa nishati inayozalishwa na tanuri la nyuklia kilichopangwa kujengwa huko Sinop, mkoa wa kaskazini wa Uturuki.

"Mvutano katika Mediterania mashariki una athari mbaya zaidi kwa Uturuki na Ugiriki, nchi mbili muhimu katika eneo hilo," Rais Erdogan alisema.

Alisisitiza haja ya mataifa yote mawili kutafuta fursa kikamilifu na kuunda manufaa ambayo yatanufaisha nchi zao huku kukiwa na changamoto zinazoendelea katika eneo hilo.

TRT Afrika