USM Alger kutoka Algeria ilishinda Kombe la Super Cup la Caf 2023 kwa kuishinda klabu ya Al Ahly ya Misri. Picha: USM Alger

Wikiendi hii ilishuhudiwa michuano mikali barani humo huku vilabu vya Afrika vikipigania kutinga hatua ya makundi ya kombe la shirikisho la CAF.

Mabingwa watetezi wa Kombe la Shirikisho la CAF, USM Alger walinusurika kwa unyoya tu wakiwa nyumbani kufuatia tisho kutoka kwa FUS Rabat katika mechi ya mashemeji wa Afrika Kaskazini na kufuzu kwa taabu.

Mchezo huo uliokuwa na upinzani mkali ulitanguliwa na sare ya 1-1 katika mkondo wa kwanza mjini Rabat.

Hata hivyo, ni mabingwa hao watetezi ambao walionyesha sifa zao za kutwaa ubingwa katika mechi ya mkondo wa pili kwa uchezaji mzuri ambao ulipelekea mchezo huo kumalizika kwa sare ya bila kufungana kwa wababe hao wa Algeria kuendelea na kampeni ya kutetea taji.

USM Alger walisonga mbele kwa sababu FUS Rabat walishindwa kufunga ugenini katika pambano la mkondo wa pili.

Washindi wa kwanza wa michuano hiyo Sekhukhune United kutoka Afrika Kusini waliwaondoa wapinzani wao Saint Eloi Lupopo kutoka DR Congo baada ya mechi kumalizika kwa sare ya 1-1 na kuwafanya Waafrika Kusini hao kutinga hatua ya makundi katika mchujo wao wa kwanza kwa jumla ya mabao 4-2.

Sekhukhune United wanashiriki kwa mara ya kwanza katika michuano hiyo. Picha: Sekhukhune United 

Rivers United ambao ni timu pekee kutoka Nigeria katika pambano la hatua ya Makundi ya CAF, walipata ushindi mnono wa mabao 2-0 wakiwa nyumbani dhidi ya Etoile Filante wa Burkina Faso na kuwafanya wasonge mbele kwa jumla ya mabao kufuatia sare ya bila kufungana ugenini katika mchezo wa kwanza.

Huko Angola, Academica do Lobito ilijihakikishia nafasi ya kufuzu kwa makundi kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 nyumbani dhidi ya Al Merreikh kufuatia sare ya bila mabao nchini Sudan.

Rivers United ambao ni timu pekee kutoka Nigeria katika pambano la hatua ya Makundi ya CAF, walipata ushindi mnono wa mabao 2-0 wakiwa nyumbani dhidi ya Etoile Filante wa Burkina Faso na kuwafanya wasonge mbele kwa jumla ya mabao kufuatia sare ya bila kufungana ugenini katika mchezo wa kwanza.

Huko Angola, Academica do Lobito ilijihakikishia nafasi ya kufuzu kwa makundi kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 nyumbani dhidi ya Al Merreikh kufuatia sare ya bila mabao nchini Sudan.

Huko Morocco, Wydad Casablanca waliendeleza ubabe wao dhidi ya Hafia Conakry kwa ushindi wa 3-0 wa mkondo wa pili, na kufanikiwa kwa jumla ya 4-1.

Kwingineko, Esperance ya Tunisia iliishinda timu ya Ivory Coast, AS Douanes kwa jumla ya mabao 1-0 na kuendelea.

Mamelodi Sundowns ilivuka kirahisi sana dhidi ya wana Burundi Bumamuru na kutinga hatua ya makundi ya CAF Champions League kwa ushindi wa jumla wa mabao 6-0.

Mchujo wa kufuzu utakamilika Jumatatu wakati timu iliyofuzu mara tatu ya robo fainali, Chabab Belouizdad ya Algeria itakapotetea uongozi wa 3-1 nyumbani dhidi ya Bo Rangers kutoka kwa Sierra Leone.

TRT Afrika