AFCON 2024 

Droo imetangazwa rasmi kwa mashindano yajayo yatakayofanyika Abidjan, Cote D'Ivoire yatakayoshuhudia walio bora zaidi barani ambao wamefuzu watakutana.

Timu zifuatazo zilitinga fainali; Algeria, Angola, Burkina Faso, Cameroon, Cape Verde, Congo DR, Misri, Equatorial Guinea, Gambia, Ghana, Guinea, Guinea-Bissau, Mali, Mauritania, Morocco, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Senegal, Afrika Kusini, Tanzania, Tunisia na Zambia.

Cote D'Ivoire ilifuzu moja kwa moja baada ya kushinda ombi la kuandaa mashindano hayo yanayofanyika kila baada ya miaka miwili. Mataifa mengine 23 yalilazimika kukata tiketi ya kucheza fainali kupitia mchujo.

Nani atakabiliana na Nani

Timu zilipangwa kulingana na viwango vyao vya Septemba FIFA.

  • Chungu cha 1: Ivory Coast, Morocco, Senegal, Tunisia, Algeria, Misri

  • Chungu cha 2: Nigeria, Cameroon, Mali, Burkina Faso, Ghana, DR Congo

  • Chungu cha 3: Afrika Kusini, Cape Verde, Guinea, Zambia, Guinea ya Ikweta, Mauritania
  • Chungu cha 4: Guinea-Bissau, Msumbiji, Namibia, Angola, Gambia, Tanzania

TRT Afrika