Wachezaji wa Galatasaray wakishangilia baada ya kutinga hatua ya makundi ya UEFA Champions League kwa ushindi wa jumla ya 5-3 dhidi ya Molde. Picha: Getty Images

Galatasaray iliishinda timu kutoka Norway ya Molde, 2-1 mjini Istanbul na kupata ushindi wa jumla ya mabao 5-3 Jumanne katika mechi ya mchujo ya UEFA Champions League, kwenye Uwanja wa Ali Sami Yeni, Istanbul.

Klabu hiyo ya Istanbul ilipata bao la uongozi kupitia mkwaju wa penalti baada ya Mauro Icardi kufunga mkwaju wa penalti dakika ya saba baada ya kuangushwa na Martin Ellingsen kwenye eneo la hatari.

Licha ya wenyeji hao kuwa mbele kwa bao la mapema kupitia penalti ya Icardi, Molde ilitoka nyuma na kusawazisha kupitia bao la Hestad kipindi cha pili.

Hata hivyo, Galatasaray ilinusurika shinikizo la dakika za lala salama kutoka kwa Molde, na kujihakikishia bao la ushindi kwenye mchezo huo kupitia kwa mkwaju uliofulululizwa na Angeliño hadi kimiani katika dakika za majeruhi.

TRT Afrika na mashirika ya habari