Gloire Bisimwa anasema alianza kupendezwa na vichekesho tangu utotoni. Picha: Bisimwa

na Kudra Maliro

Lakini Gloire Bisimwa ana njia yake ya kuwapa watu furaha na kuhimiza kuishi pamoja kwa amani.

Ndani kabisa ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambako makundi yenye silaha yamesababisha uharibifu mkubwa kwa mashambulizi kwenye vijiji na kambi za kijeshi, mcheshi mwenye umri wa miaka 23 amekuwa akiandaa njia ya amani kupitia vichekesho.

Gloire Bisimwa amekuwa akisambazwa sana na watumiaji wa Tik Tok kutoka Kongo kwa kutumia sanaa zake zinazomwiga Charlie Chaplin, mwigizaji-mchekeshaji maarufu wa Kiingereza aliyefariki mwaka wa 1977.

Wafuasi wa Gloire Bisimwa wanamwona kuwa 'zawadi kutoka kwa Mungu'. Picha: Bismwa

"Tangu nikiwa mtoto, nimefuatilia filamu za vichekesho vya Charlie Chaplin na ilinipa furaha kubwa kuona vitendo hivyo. Ninapenda jinsi anavyowachekesha watu," kijana huyo mwenye umri wa miaka 23, aliyempa jina la utani la Charlie Chaplin wa Kongo. aliiambia TRT Afrika.

Nakumbuka mama yangu aliniambia nioge kabla ya kuona filamu za Charlie na napenda jinsi anavyowachekesha watu,

Mashariki mwa Kongo kumekuwa eneo la mzozo mbaya kwa zaidi ya miaka 30, na vijana wengi katika eneo hilo wanatumia dawa za kulevya ili kukabiliana na matatizo ya kiakili ya vita. Baadhi yao wanavutiwa na vikundi vyenye silaha vinavyowasajili.

Ujumbe wa Amani

Mashabiki wanasema sanaa ya Gloire Bisimwa inaleta furaha huku kukiwa na dhiki ya mizozo ya kivita. Picha: Bismwa

Gloire alisema anatumia mamia ya dola kununua mavazi ya ukumbi wa michezo ili kufanana na Charlie Chaplin.

"Ninaagiza suti kutoka Kinshasa (mji mkuu) na mara nyingi mimi hutengeneza nguo mwenyewe," anasema mcheshi huyo.

“Mbali na mitandao ya kijamii, ningependa pia kuandaa maonyesho zaidi makanisani, mitaani na ulimwenguni kote ili kufikisha ujumbe wa amani na kuleta furaha,” anaongeza.

Charlie Chaplin alikuwa nyota wa filamu za uchekeshaji ambaye alivutia umakini wa ulimwengu wote katika jukumu la Jambazi Mdogo katika filamu zake kati ya 1914 na 1936.

TRT Afrika