Wananchi Zimbabwe wanapiga kura kuchagua rais na viongozi wengine / picha : AFP 

Takriban watu milioni sita na laki sita walijiandikisha kupiga kura katika taifa hilo lenye idadi ya takriban watu milioni 15.

Rais wa sasa Mnangagwa anagombea kiti kwa awamu ya pili na ya mwisho / Picha: Others

Akipiga kura yake katika mji alikozaliwa wa Kwekwe, katikati mwa Zimbabwe, rais wa sasa Emmerson Mnangagwa anayegomea kiti kwa awamu ya pili, aliwaambia waandishi wa habari,

"Kama nadhani sitachukua, basi nitakuwa mjinga."

Nelson Chamisa ndiye mpinzani mkuu wa rais Mnangagwa / Picha: AFP

Nelson Chamisa mgombea mwingine anaonekana kama mpinzani mkuu wa rais Mnangangwa.

Zaidi ya watu milioni sita walijisajili kupiga kura / Picha: Reuters 

Matokeo ya ubunge yanatarajiwa kuanza kutangazwa kufikia Alhamisi asubuhi. Matokeo ya urais yanatarajiwa kuja baadaye, ingawa ni ndani ya siku tano.

Watu walijitokeza katika sehemu tofauti nchini kupiga kura / Picha: Others         

Ili kushinda urais, mgombea lazima apate zaidi ya 50% ya kura.

Ikiwa hakuna mshindi wa moja kwa moja, marudio ya uchaguzi yatafanywa kati ya wagombea wawili wa juu yatafanyika Oktoba tarehe 2.

Wananchi wanalalamikia gharama ya juu ya maisha /Picha:Others 

Wagombea wa kura za udiwani wanahitaji puta wingi wa kura zilizopigwa ili kutangazwa washindi

TRT Afrika