Bendera ya Tunisia. / Pıcha: Getty / Photo: Getty Images

Harakati ya Nahda imetangaza kupitia tovuti yake ya mtandao wa kijamii kuwa Makamu Mwenyekiti wake Munsir al-Venisi alizuiliwa na vikosi vya usalama siku ya Jumanne jioni na kupelekwa eneo lisikojulikana.

Vuguvugu la Nahda, linalotaka kuachiliwa kwa Makamu wake wa Rais Venisi, lilibainisha kuwa wanasimama vikamilifu na Venisi.

Mkuu wa Baraza la Shura la Vuguvugu hilo, Abdulkarim al-Haruni pia ni miongoni mwa waliozuiliwa.

Riyad al-Shuaibi, Mshauri wa Kisiasa wa Kiongozi wa Harakati ya Nahda Rashid al-Ghannouchi, alichapisha kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, kuwa "Abdulkarim al-Haruni, Mwenyekiti wa Baraza la Harakati ya Nahda Shura, sasa amezuiliwa."

Ingawa Shuaybi hakutaja sababu za kuzuiliwa kwa Haruni, alieleza kuwa Venisi, ambaye aliwekwa kizuizini hapo awali, atazuiliwa na Kurugenzi ya Kupambana na Uhalifu wa Kielektroniki kwa saa 48.

Waziri Mkuu wa zamani wa Tunisia Hammadi al-Jibali ambaye pia ni Mwanachama mwingine wa zamani wa Nahda, alichukuliwa na vikosi vya usalama kutoka nyumbani kwake katika mji wa Susa, kusini mwa mji mkuu wa Tunis, jana asubuhi na kuachiliwa na ofisi ya mwendesha mashtaka baada ya kuhojiwa kwa saa 7.

Spika wa zamani wa Bunge la Tunisia Rashid al-Ghannouchi, na pia Kiongozi wa vuguvugu hilo, alikamatwa Aprili 17 baada ya polisi kuvamia nyumba yake kwa madai ya "kuwaongoza watu kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe" na alikamatwa baada ya mahojiano ya saa 48 na polisi. Ghannouchi anaendelea kuzuiliwa.

Kukamatwa kwa wanasiasa nchini Tunisia

Tangu Februari 11, operesheni zinazohusisha kuwafunga wanasiasa, waandishi wa habari, wanaharakati, majaji na wafanyabiashara zimekuwa zikifanyika nchini Tunisia. Wapinzani wengi waliwekwa gerezani kupitia operesheni hizi.

Aidha, mwishowe tarehe 3 Septemba, Abdulkarim al-Haruni, Mwenyekiti wa Baraza la Shura la Nahda, aliwekwa chini ya kizuizi cha nyumbani.

Akizungumzia hatua za kukakamatwa kwa wapinzani, Rais wa Tunisia Qays Saeed alisema katika taarifa yake kwamba kufungwa kwa wanasiasa ilitekelezwa kwa sababu ya "kupanga njama dhidi ya usalama wa serikali" na hatua zinazolenga kuchochea mzozo wa kiuchumi.

Upinzani unaita uchunguzi huo kuwa wa kisiasa na unamtuhumu Saeed kwa kutenda kinyume na demokrasia.

AA