Serikali ya Somalia hivi karibuni imeomba msaada wa Kimataifa ili kuzuia kuzuka upya kwa uharamia/ Picha wengine

Jeshi la polisi wa wanamaji wa Somalia liliimarisha doria katika Bahari Nyekundu kufuatia kushindwa kuteka nyara meli katika Ghuba ya Aden mapema wiki hii.

Kamanda wa kikosi cha wanamaji katika eneo la Puntland, Abdullahi Mohamed Ahmed, alisema kwamba doria katika maji imeongezeka maradufu na walikuwa kwenye mzunguko wa saa 24 ili kuwazuia maharamia.

“Hapa sasa tuna changamoto nyingi. Hapo awali tulishughulika na maharamia na kusimamisha shughuli zao."

Serikali ya Somalia hivi karibuni imeomba msaada wa Kimataifa ili kuzuia kuzuka upya kwa uharamia.

Somalia kwa miaka mingi ilikumbwa na uharamia, huku kilele kikiwa 2011, wakati Umoja wa Mataifa uliposema kuwa zaidi ya mashambulizi 160 yalirekodiwa katika pwani ya Somalia.

Matukio hayo yamepungua kwa kiasi kikubwa tangu wakati huo.

TRT Afrika