Baadhi ya sanaa hizo zikiwa kwenye maonesho katika mkutano huo wa Kidiplomasia :Picha/ TRT Afrika

Na Coletta Wanjohi

Mkutano wa Kidiplomasia wa Antalya uliwaleta pamoja wakuu wa nchi na serikali, mawaziri, wanadiplomasia, wafanyabiashara, wanazuoni huku majopo na maonesho mbalimbali yaliyoangazia masuala ya siasa, uchumi, elimu na utamaduni yakitamalaki.

Maonesho ya Afrika yapamba mkutano wa Kidiplomasia wa Antalya./Picha: TRT Afrika

Mkutano huo uliofanyika katika mji wa pwani wa Antalya, kando ya bahari ya Mediterenia, ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka zaidi ya nchi 140, nyingi zikiwa ni za kiafrika.

Moja ya vivutio vya mkutano huo ni kazi za mikono zilizowakilisha utamaduni wa kiafrika.

Baadhi ya kazi za sanaa kutoka Afrika, ndani ya mkutano wa Kidiplomasia wa Antalya. /Picha: TRT Afrika

Kongamano hilo la Kidiplomasia la Antalya lilitoa fursa ya kubadilishana tamaduni kati ya watu kutoka mataifa mbalimbali duniani, kupitia kazi za sanaa.

Kongamano hilo lilitoa fursa ya kubadilishana tamaduni kati ya watu kutoka mataifa mbalimbali. Picha:/ TRT Afrika

Ufinyanzi, ufundi wa chuma, uchongaji, usanifu, sanaa ya nguo ni baadhi ya aina za sanaa za maonyesho katika nchi za Afrika.

Baadhi ya sanaa katika mkutano wa Antalya. /Picha: TRT Afrika

Aina za sanaa hii huipa Afrika utambulisho wa kipekee na urithi wa watu wake.

Sanaa ya Afrika./Picha:TRT Afrika

Wageni wengi walipata muda wa kutazama na kufurahia maonesho mbalimbali katika mkutano wa Kidiplomasia wa Antalya.

Sanaa kutoka Afrika./Picha:TRTAfrika

Mkutano wa mwaka huu ulikuwa na matukio tofauti ikiwemo majopo, maonesho ya sanaa na teknolojia.

TRT Afrika