Murat Karayilan, anayejulikana pia kama Cemal, ni mmoja wa waanzilishi wa shirika la kigaidi la PKK/ Picha Wengine 

Gaidi Yunus Aras, anayejulikana pia kwa jina la siri Herekol Hezex ambaye aliwahi kuwa mlinzi wa kiongozi wa PKK Murat Karayilan, amekatwa makali, vikosi vya Uturuki, Waziri wa Mambo ya Ndani alitangaza.

Akitoa taarifa kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii siku ya Ijumaa, Ali Yerlikaya alisema Aras alikuwa miongoni mwa wanachama wawili wa PKK waliokuwa chini ya uangalizi katika eneo la kitongoji cha Alayurt katika wilaya ya Dargecit mkoa wa Mardin na Kikosi cha usalama cha Mkoa wa Mardin.

"Kwa kuratibiwa na Kurugenzi ya Ujasusi ya Kamanda Mkuu wa kikosi cha jeshi, magaidi walikatwa makali katika operesheni ya 'Heroes-32' mnamo Desemba 4," alisema.

Katika uchunguzi wa DNA wa mwanachama asiyejulikana wa PKK ambaye alikatwa makali, ilibainika kuwa mtu huyo alikuwa Yunus Aras, Yerlikaya aliongeza.

Ilibainika kuwa gaidi huyo alishiriki katika jumla ya mashambulizi manne, na kusababisha vifo vya askari wanne wa usalama na wengine 15 kujeruhiwa, kama alivyosema waziri.

Gaidi Murat Karayilan ni nani?

Murat Karayilan, anayejulikana pia kama Cemal, ni mmoja wa waanzilishi wa shirika la kigaidi la PKK. Anaangazia orodha ya "magaidi wanaosakwa zaidi" na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uturuki.

Baada ya kujiunga na PKK mwaka wa 1979, alikua kiongozi mkuu wa kundi hilo la kigaidi baada ya kiongozi wake wa itikadi kali, Abdullah Ocalan, kukamatwa na maafisa wa kijasusi wa Uturuki mwaka 1999.

Uongozi wa shirika hilo la kigaidi ulihamia eneo la milima la Qandil la Iraq muda mfupi baadaye.

Ofisi ya Marekani ya Udhibiti wa Mali za Kigeni (OFAC) ilitangaza kwamba ilimhesabu Karayilan miongoni mwa "walanguzi wakubwa wa mihadarati wa kigeni" katika mwaka huo huo alipochukua utawala wa PKK.

Karayilan aliteuliwa kama kamanda mkuu mpya wa HPG, mrengo wa kijeshi wa PKK, mnamo 2014.

Mnamo Desemba 13, 2016, mwendesha mashtaka mkuu wa mkoa wa Mardin wa Uturuki pia alitoa vibali vya kukamatwa kwa Karayilan na Duran Kalkan, kamanda mwingine wa PKK, kufuatia mauaji ya Gavana wa Wilaya ya Derik Muhammet Fatih Safiturk, 35, katika ofisi yake na vilipuzi vilivyotengenezwa kwa mkono.

Safiturk alikuwa ameteuliwa hivi majuzi kama meya wa wilaya hiyo baada ya meya wa awali kuzuiliwa, akikabiliwa na mashtaka ya kuwa na uhusiano na PKK.

Uongozi wa shirika hilo la kigaidi ulihamia eneo la milima la Qandil ya Iraq muda mfupi baadaye.

Ofisi ya Marekani ya Udhibiti wa Mali za Kigeni (OFAC) ilitangaza kwamba ilimhesabu Karayilan miongoni mwa "walanguzi wakubwa wa mihadarati wa kigeni" katika mwaka huo huo alipochukua utawala wa PKK.

Karayilan aliteuliwa kama kamanda mkuu mpya wa HPG, mrengo wa kijeshi wa PKK, mnamo 2014.

Safiturk alikuwa ameteuliwa hivi majuzi kama meya wa wilaya hiyo baada ya meya wa awali kuzuiliwa, akikabiliwa na mashtaka ya kuwa na uhusiano na PKK.

TRT Afrika