Rais wa DRC ataja mauaji ya mbunge huyo wa upinzani kuwa ya kudharauliwa. Picha: AFP

Mbunge wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alipatikana amefariki Alhamisi katika mji mkuu Kinshasa, chama chake na wanafamilia walisema.

Cherubin Okende, waziri wa zamani wa uchukuzi katika serikali ya Rais Felix Tshisekedi, alipatikana amefariki ndani ya gari lake akiwa na majeraha ya risasi, kulingana na familia.

Waziri wa Mawasiliano wa Kongo na msemaji wa serikali Patrick Muyaya alisema serikali "ilipata habari kwa masikitiko makubwa na hofu juu ya mauaji" ya Okende.

Ofisi ya rais ilisema Rais Tshisekedi alijifunza kwa kusikitishwa na "kutoweka katika hali mbaya" ya Okende.

“Mkuu wa nchi anatoa risala zake za rambirambi kwa familia na wapendwa wa Mheshimiwa Okende. Anahimiza Haki kuangazia kesi hii ili kuwaadhibu wahalifu wa kitendo hiki cha kudharauliwa,” ilisema ofisi ya rais kwenye Twitter.

Uchaguzi mbele

Okende, 62, alikaimu nafasi ya msemaji wa chama cha upinzani (Together for the Republic party,) ambacho kiongozi wake, Moise Katumbi, ametangaza nia yake ya kugombea katika uchaguzi wa urais unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Alijiuzulu kutoka kwa serikali ya Tshisekedi Desemba mwaka jana pamoja na mawaziri wengine wawili waliokuwa katika muungano unaotawala.

Katumbi alilaani kifo hicho, akikitaja kuwa ni "mauaji ya kisiasa yenye lengo la kutunyamazisha."

"Uchunguzi huru lazima ufanywe ili kutoa mwanga juu ya kile kinachoonekana kama uhalifu wa serikali," alisema.

Ripoti zilisema Okende alitoweka mapema Jumatano. Chama chake kilisema alitekwa nyara katika eneo la kuegesha magari la Mahakama ya Kikatiba.

Kifo chake kinakuja huku kukiwa na hali ya wasiwasi ya kisiasa kabla ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwezi Disemba.

TRT Afrika