Matokeo ya uchaguzi wa rais wa DRC yanatarajiwa leo

Matokeo ya uchaguzi wa rais wa DRC yanatarajiwa leo

Kwa kiasi fulani kufikia hadi sasa Rais Felix Tshisekedi anaongoza
Uchaguzi ulifanyika Desemba 20. Picha: TRT Afrika

Tume ya uchaguzi ya kitaifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (CENI) inatarajiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais ya Desemba 20 Jumapili ya leo, tarehe 31 Desemba.

Hesabu za mpaka sasa zinaonyesha Rais Felix Tshisekedi akiwa ana ongoza, ingawa upinzani umetoa wito wa kurudiwa kwa uchaguzi.

Tshisekedi, mwenye umri wa miaka 60, amekuwa madarakani tangu Januari 2019 na anagombea muhula wa pili wa miaka mitano. Ifikapo Jumamosi jioni, kwa kura milioni 17.8 zilizohesabiwa, alikuwa anaongoza kwa asilimia 72.

Moise Katumbi, mfanyabiashara na aliyekuwa gavana wa mkoa wa Katanga kusini-mashariki, alikuwa wa pili kwa asilimia 18.9.

Marufuku ya Maandamano

Martin Fayulu alikuwa anafuata kwa asilimia 5.5, na waziri mkuu wa zamani Adolphe Muzito alikuwa na asilimia 1.36.

Baadhi ya wagombea wa upinzani walikuwa wamepanga maandamano dhidi ya matokeo ya uchaguzi wiki iliyopita wakidai kuwepo kwa udanganyifu. Polisi walizuia maandamano hayo.

Watu takriban milioni 44 kati ya wakazi milioni 100 wa nchi kubwa walikuwa wamesajiliwa kupiga kura Desemba 20 kwa rais, pamoja na wabunge wa kitaifa na wa kikanda na madiwani wa manispaa.

Awali ilipangwa kufanyika Desemba 20, upigaji kura uliongezwa rasmi kwa siku moja ili kufidia matatizo ikiwa ni pamoja na ucheleweshaji katika baadhi ya vituo.

Wito wa Kujizuia

Upigaji kura uliendelea kwa siku kadhaa baadaye katika baadhi ya maeneo ya mbali, kulingana na waangalizi. DRC ni nchi ya pili kwa ukubwa barani Afrika kwa eneo.

Ubalozi takriban 15 umetoa wito wa "kujizuia" katika nchi tajiri kwa madini kabla ya kutangazwa kwa matokeo.

Mamlaka zinasema zimechukua hatua za kuzuia machafuko, hasa katika maeneo ya madini ya kusini-mashariki.

Pia zinasistiza kwamba migogoro yoyote ya uchaguzi lazima iwasilishwe kwa Mahakama ya Katiba, ambayo itatangaza matokeo ya mwisho, yanayotarajiwa Januari 10.

TRT Afrika