Takwimu za Benki Kuu ya Tunisia (BCT) zinaonyesha kuwa taifa hilo lilikusanya Dinari ya Tunisia bilioni 1.7 (dola milioni 549.8) / Picha: Getty  / Photo: Getty Images

Mapato ya utalii nchini Tunisia yameongezeka kwa asilimia 57.7 katika miezi mitano ya kwanza ya 2023.

Takwimu za Benki Kuu ya Tunisia (BCT) zinaonyesha kuwa taifa hilo lilikusanya Dinari ya Tunisia bilioni 1.7 (dola milioni 549.8) kutokana na utalii ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2022.

Wakati huo huo, kodi ya mapato ilipanda kwa asilimia 6 hadi bilioni 3.1 Dinari ya Tunisia (dola bilioni 1) kati ya Januari na Mei 2023.

Benki kuu ilisema mzigo wa deni la nje ulipungua kwa asilimia 10, kutoka Dinari ya Tunisia bilioni 3.6 (dola bilioni 1.16) kati ya Januari na Mei mwaka jana hadi Dinar 3.2 ya Tunisia (dola bilioni 1.03) katika kipindi kama hicho mwaka 2023.

Akiba ya fedha za kigeni ya Tunisia pia ilishuka kwa Dinari ya Tunisia bilioni 3.1 (dola bilioni 1.9) katika kipindi hicho, kutoka bilioni 24.4 (dola bilioni 7.9) mwaka 2022.

Zaidi ya watalii milioni moja walikuwa wametembelea Tunisia katika miezi mitano ya kwanza ya 2023.

Katika mwaka mzima wa 2022, Tunisia ilirekodi wageni milioni 6.3 waliofika, rekodi rasmi zilionyesha.

Ufaransa, Ujerumani, Poland, Czech na Algeria ndizo nchi zilizochangia idadi kubwa ya wageni wa Tunisia.

Utalii ni nguzo muhimu ya uchumi wa Tunisia, ikiwakilisha asilimia 14 ya pato la taifa (GDP).

Pia inatoa karibu ajira 400,000 za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja Tunisia.

Jiji la kale la Carthage, ukumbi wa michezo huko El Djem, Makumbusho ya Kitaifa ya Bardo, Jangwa la Sahara na Jiji la Kale la Dugga ni kati ya maeneo maarufu ya vivutio vya watalii nchini.

TRT Afrika