Rais Nana Akufo-Addo alibainisha kwamba marekebisho hayo ni juhudi za kuboresha utoaji wa huduma ya afya ya akili nchini / Photo: Reuters

Watetezi wa afya ya akili wa Ghana wameuita uamuzi wa mamlaka ya Ghana wa kuharamisha kujiua kuwa vita vikali vilivyobeba ushindi.

Ghana hivi karibuni ilifanyia marekebisho Sheria ya Makosa ya Jinai ya 1960, ambayo hapo awali ilifanya jaribio la kujiua kuwa kosa la jinai nchini humo.

Marekebisho hayo mapya sasa yanasema kuwa jaribio la kujiua litazingatiwa kuwa suala la afya ya akili linalohitaji usaidizi wa sheria badala ya uhalifu.

Kabla ya marekebisho hayo, yeyote aliyepatikana na hatia ya kujaribu kujiua anaweza kuhukumiwa kati ya miezi mitatu na miaka miwili.

Profesa Akwasi Osei, ambaye alikuwa mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Afya ya Akili ya Ghana, aliiita afueni kubwa.

''Tuna furaha kuhusu sheria hii iliyorekebishwa ambayo imekuwa ikiwafunga watu kwa kuwa na matatizo ya afya ya akili. Mielekeo ya kutaka kujiua ni hali ya afya ya akili.'' Osei anaiambia TRT Afrika.

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, karibu watu 700,000 hujiua kila mwaka ulimwenguni. Kwa kila kujiua kukamilika, kuna angalau majaribio 20 yasiyofaulu.

Rais Nana Akufo-Addo alibainisha katika uzinduzi wa jengo la magonjwa ya akili la Hospitali ya Korle-Bu Teaching mjini Accra kwamba marekebisho hayo ni juhudi za kuboresha utoaji wa huduma ya afya ya akili nchini.

Profesa Osei alisema nchi ambazo bado zinatoa adhabu ya uhalifu wa kujiua lazima zifikirie upya.

''Siyo haki. Ni kana kwamba wanaadhibiwa kwa kutokamilisha jaribio la kujitoa uhai kwa sababu ndivyo sheria hii inalenga. Inalenga jaribio la kujiua. Waathiriwa wa hali hii wanahitaji tu msaada. Hawapaswi kuadhibiwa kwa hilo.''

Ghana, India, Kuwait, Nigeria, Pakistan, Rwanda, na Singapore ni nchi mashuhuri zinazotumia kanuni hii ya adhabu.

Kulingana na Taasisi ya Kitaifa ya Afya ya Ghana, takriban visa 1,500 vya kujitoa mhanga huripotiwa kila mwaka nchini humo.

TRT Afrika