Muhogo husindikwa na kuliwa kwa njia mbalimbali barani Afrika. Picha: Reuters

Na Firmain Eric Mbadinga

Karne kadhaa baada ya kuagizwa kwa mara ya kwanza barani Afrika, ikiripotiwa kutoka Amerika ya kitropiki, haishangazi kwamba mihogo sasa imekita mizizi katika vyakula vya kitamaduni vya jamii katika sehemu nyingi za bara.

Mmiliki wa mgahawa, Éliane Obiyi, mzaliwa wa jimbo la Haut-Ogooué nchini Gabon, ni miongoni mwa mamilioni ya Waafrika waliojumuisha mihogo katika karibu kila ain aya chakula anachopika.

Kama mtu aliyefunzwa katika huduma ya afya, anajali sana kile kinachoingia kwenye chakula chake, na mihogo katika aina zake zote inaonekana kuendana na mtindo wake wa maisha.

Mizizi ya muhogo iliyochukuliwa kutoka ardhini husagwa kwenye mashine. Picha: TRT Afrika

"Miongoni mwa mazao mbalimbali ya kilimo ninayopendelea kutumia, muhogo unapata fahari ya mahali pake kwa sababu unaweza kusindika kwa njia tofauti. Pia ni muhimu kwa utamaduni wetu wa Kiafrika," anaiambia TRT Afrika.

Éliane alianza safari yake ya kibiashara na upishi kwa kuuza vyakula vya mabanda mitaani. Alijiendeleza hadi kufungua huduma yakupelekea wateja ake chakula nyumbani kabla ya kufungua mkahawa wake huko Franceville, mji mkuu wa mkoa wa Haut-Ogooué.

Katika hatua zote hizi za biashara yake, utayarishaji wa zao hili la mizizi unategemea mbinu alizojifunza kutoka kwa wazazi wake. Anaendelea kuboresha taratibu hizi, akitoa vyakula vya kibunifu na mihogo kama kiungo kikuu.

"Dokô, au manioc obamba, hutengenezwa kwa kuloweka kiazi chungu cha muhogo katika maji mengi kwa siku kadhaa ili kulainisha," anaelezea Éliane.

Sima ya Mhogo au maarufu kama foufou upande wa Afrika Magharibi / Picha : TRT Afrika

“Baada ya hapo huchujwa na kusagwa kwenye mashine hadi upatikane rojo lake, baada ya awamu hii mihogo ichemshwe pembeni, hatua ya mwisho ni kuufunga mchanganyiko huo uliokwisha kupikwa kwenye karatasi ya kitamaduni na kuoka kwa takribani dakika 20."

Vyakula mbali mbali

Kando na Doko, inayoliwa sana nchini Gabon na nchi nyinginezo kama vile Cameroon, Guinea, DR Congo na Jamhuri ya Kongo pamoja na Angola, Attiéké ni aina nyingine maarufu ya kiazi cha muhogo.

''Ili kutengeneza Attiéké, lazima uchukue kiazi moja kwa moja kutoka ardhini, uoshe, na ukipondaponda kwenye mashine. Mara baada ya kusagwa, unapaswa kukamua 90% ya maji yake. Baada ya hatua hii, chuja mguu wa kiazi na upike siku hiyo hiyo, "anasema Éliane.

"siri ni kuikoroga mara kwa mara juu ya moto mdogo ili kuizuia kuganda katika sufuria, na kisha ikauke kwenye sufuria yenye maji kwa takriban dakika tano."

Njia nyingine ya kupika mizizi ya manioc, ambayo majani yake pia yanaweza kuliwa, ni Gari. Hii inafanywa kwa njia sawa na Attiéké, isipokuwa moja.

Éliane Obiyi ni mfanyakazi wa afya aliyefunzwa. Picha: TRT Afrika.

"Tofauti kati ya Gari na Attiéké ni baada ya hatua ya kuchuja. Bidhaa zote mbili hupondwa kwenye mashine, kung'olewa, na kuchujwa. Hata hivyo, tofauti na Attiéké, ambayo inapaswa kupikwa mara moja baadaye, Gari hupatikana kwa kukausha mguu unaosababishwa kwenye jua kwa siku kadhaa," anasema Éliane.

Gari mara nyingi huliwa kama nafaka na maziwa na sukari au hupikwa kwa maji na mafuta na chumvi kidogo.

Mkulima wa muhogo katika mji mkuu wa Cote d'Ivoire Yamoussoukro. Picha: Reuters

Kama vile Attiéké, Doko na Gari ni maarufu, haswa katika Afrika Magharibi na Kati, Foufou ni maarufu sana. chakula hiki, ambachao pia huitwa Fufu, hutengenezwa kwa kuchemsha unga wa muhogo na mara nyingi hutumika kama kiambatanisho cha vyakule vingine vya mchuzi.

Kama mhudumu wa chakula, Éliane anasema amegundua kupendezwa zaidi na Dokô miongoni mwa wateja wake na anafaidika nayo. "Bado nina uzoefu wa kupata, lakini biashara hii ina faida kubwa na hatimaye itaniwezesha kujitegemea kifedha."

Kwa hatua inayofuata ya biashara yake, inayojumuisha huduma nyingi zaidi za upishi, Éliane ana ndoto ya kuliteka jimbo lake la nyumbani kwa vyakula mbalimbali vya mihogo na kisha kuweka macho yake huko Libreville, mji mkuu wa Gabon, ambako kuna mahitaji makubwa ya kiazi hicho katika hali tofauti.

Bei za muhogo nchini Gabon huanzia 500 CFA franc na kwenda juu kwa kijiti cha 500gm. Vivyo hivyo kwa Foufou, Gari, na majani ya mihogo, ambayo hutumiwa kama mboga.

TRT Afrika