Milio ya risasi karibu na Jumba la Kitaifa la Haiti, huko Port-au-Prince / Picha: Reuters

Hali nchini Haiti ni "maangamizi makubwa," ambapo zaidi ya watu 1,500 wameuawa kutokana na ghasia za magenge mwaka huu na silaha zaidi zinaendelea kumiminika nchini humo, Umoja wa Mataifa ulisema Alhamisi.

Katika ripoti mpya, ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ilielezea jinsi "ufisadi na utawala mbovu, pamoja na ongezeko la viwango vya ghasia za magenge (vilivyo) dhoofisha utawala wa sheria na kuleta taasisi za serikali... karibu na kuanguka."

Hii, ilisema, imeiacha Haiti katika "hali ya maangamizi makubwa."

Haiti, ambayo imekumbwa na ghasia kwa muda mrefu, imegubikwa na mapigano yanayoongezeka tangu mwishoni mwa Februari wakati magenge yalipozindua mashambulizi iliyoratibiwa na kudai Waziri Mkuu Ariel Henry ajiuzulu.

Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu

Henry, ambaye ameongoza Haiti tangu mauaji ya Rais Jovenel Moise mwaka 2021, aliahidi zaidi ya wiki mbili zilizopita kujiuzulu baada ya baraza la mpito kuanzishwa - ingawa kufikia hatua hiyo imekuwa vigumu sana kutokana na mizozo kati ya viongozi wa vyama.

Wakati huo huo, idadi ya waathiriwa inaongezeka.

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ilibaini kwamba ghasia za magenge zilisababisha vifo vya watu 4,451 na wengine 1,668 kujeruhiwa mwaka jana.

Na tu katika miezi mitatu ya kwanza ya 2024 pekee, hadi Machi 22, watu 1,554 waliuawa na 826 kujeruhiwa, ilisema.

AFP