Erdoğan katika sherehe ya utoaji wa nyumba mpya zilizojengwa kwa waathirika wa tetemeko la Ardhi Huko Gaziantep. / Picha: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amezuru eneo lililoathiriwa na matetemeko ya ardhi ya Februari 6, 2023, na kutoa nyumba mpya kwa raia walioathiriwa na matetemeko hayo kama kumbukumbu huku ikikaribia kutimia mwaka mmoja tangu janga hilo.

"Uturuki inaponya haraka majeraha ya janga la karne kwa kuonyesha mshikamano wa karne," Erdogan alisema, akihutubia sherehe muhimu ya kukaboidhi nyumba 10,698 za baada ya tetemeko huko Gaziantep, siku ya Jumapili.

Akikumbuka kwa huruma zaidi ya raia elfu 53 waliopoteza maisha katika matetemeko ya ardhi, rais alisisitiza kwamba mamlaka zimekuwa zikifanya kazi bila kukatizwa kujenga upya eneo la tetemeko la ardhi.

Huko Gaziantep pekee, ujenzi wa karibu nyumba elfu 14 unaendelea haraka.

Erdogan pia alihudhuria sherehe ya ufunguzi wa Hospitali ya Jiji La Gaziantep, ambapo aliapa kuwa Uturuki "haitapumzika hadi tutakapofufua kabisa miji yetu iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi na miundombinu yao, muundo wa juu, vituo vya jiji na maeneo ya vijijini.”

Mnamo Ijumaa, Erdogan alikuwa Hatay, mji ulioathiriwa zaidi na janga hilo, ambapo idadi kubwa zaidi ya vifo ilitokea.

Katika siku zijazo, atatembelea Kahramanmaras, Sanliurfa, Adiyaman, na Elazig kuhudhuria sherehe muhimu za uzinduzi.

Kufufua miji iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi

Matetemeko ya ardhi ya Februari 6, 2023, yaligonga wilaya 124 na vijiji elfu 7 na vitongoji vya miji 11, na kuathiri watu milioni 14 na huku zaidi ya watu elfu 53 wakifariki.

"Pamoja na ujenzi wa maeneo mapya ya makazi na mabadiliko ya mitandao huko Hatay na miji mingine iliyoathiriwa na tetemeko, tutawapa wamiliki wote halali nyumba zao au mahali pa kazi," Erdogan alisema Ijumaa, akihutubia sherehe muhimu ya makabidhiano ya nyumba za baada ya tetemeko huko Hatay.

"Raia wetu wanaweza kuwa na uhakika na kutuamini sisi na serikali yao juu ya suala hili," aliongeza.

Jumla ya nyumba 7,275 za baada ya tetemeko la ardhi zilikabidhiwa wamiliki wao katika sherehe hiyo.

Akizungumza baadaye wakati wa ufunguzi wa Hospitali ya Mafunzo na Utafiti, Hatay na Hospitali ya Umma ya Iskenderun, Erdogan alielezea kuwa walikuwa wakilenga kufufua, haraka iwezekanavyo, miji yote iliyoathiriwa na tetemeko la Ardhi, haswa Hatay.

TRT World