Kuhusu mchakato wa Uturuki kujiunga na Umoja wa Ulaya, EU, Rais wa Uturuki Erdogan amesema Ankara itatathmini maendeleo na "inaweza kuachana na EU iwapo italazimika." / Photo: AA      

Uturuki imependekeza kuongoza mazungumzo ya pande tatu kuhusu Karabakh la Azerbaijan, linalohusisha nchi mbili hizo na jirani Armenia, huku akionyesha utayari wake wa mazungumzo ya njia nne yatakayohusisha Urusi, amesema Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

"Tumewasilisha pendekezo letu kwa mkutano wa pande tatu chini ya uongozi wetu kwa wao, (Azerbaijan na Armenia). Mbali na njia ya maongezi ya pande tatu, pia tumetoa pendekezo la maongezi ya pande nne," Erdogan amesema katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Istanbul siku ya Jumamosi akijiandaa kuondoka kwa ajili ya mkutano wa wiki ijayo wa Umoja wa Mataifa huko jijini New York, Marekani.

"Bado hakujakuwa na majibu," amesema kuhusu pendekezo la pande nne, akisema kwamba atajadiliana jambo hilo na rais mwenzio wa Azerbaijani Ilham Aliyev.

Kuhusu Uturuki kujiunga na Umoja wa Ulaya, Erdogan amesema Ankara itafanya tathmini ya maendeleo ya hivi karibuni. "Baada ya tathmini hiyo, tutaachana na EU kama kuna ulazima."

Umoja wa Ulaya "unajaribu kujitenga" na Ankara, amesema katika ripoti ya Bunge la Ulaya ya mwaka 2022 kuhusu Uturuki.

Kuhusu ombi la Sweden kuwa mwanachama wa NATO, amesema iwapo magaidi wanaruhusiwa kufanya maandamano chini ya ulinzi wa polisi katika nchi ya Scandinavia, hii inaonyesha kwamba Stockholm ilishindwa "kutimiza wajibu wake" chini ya makubaliano na Ankara kutoa mwanga wa kujiunga na umoja huo.

TRT World